Mwanamuziki Nguza Viking (Babu Seya) pamoja na Mwanaye Papii Kocha wakipunga mikono muda huu baada ya kutoka katika Gereza la Ukonga jijini Dar es salaam wakokuwa wanatumikia kifungo cha maisha na sasa wameachiwa huru kwa msamaha wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli alioutoa leo huko Mjini Dodoma kulikofanyika Maadhimisho ya miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania Bara. Babu Seya na Mwanawe ni sehemu ya wafungwa 8157 walipata msamaha wa Rais.
Babu Seya akitoka gerezani jioni hii.
Baadhi ya mashabiki wa wanamuzi wakiwa nje ya gereza la Ukonga Dar es Salaam wakimsubiri mwanamuziki Nguza Viking na mtoto wake Papi Kocha waliokuwa wanatumikia kifungo cha maisha jela na sasa wamepata msamaha. Picha na Said Mwinshehe, Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...