Na Kajunason/MMG.
Mkuu
wa Wilaya ya Same, Rosemary Senyamule amewataka wasimamizi wa mpango wa
Ufuatiliaji wa Matumizi ya Umma (PETS) kuwa na uadilifu katika
kufiatilia matumizi ya fedha za serikali.
Hayo ameyazungumza leo wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo
uliowakutanisha viongozi wa serikali, dini na wasimamizi wa mpango wa
"Public Expenditure Tracking System" (PETS) uliofanyika Same kwa
kuwezeshwa na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT).
Mhe.
Senyamule alisema ni vyema watendaji hao wakafuata misingi imara
itakayowezesha serikali kujua ni wapi wanamatumizi mabovu ya fedha
katika halmashauli.
Aliagiza halmashauri kushirikiana kwa karibu na watu hao kwani kazi
wanayoifanya ni ya halmashauri, hasa ukaguzi na mipango. "Idara ya
ukaguzi ina watumishi 3 tu wanaohitaji kukagua kila kitu, sio rahisi
wakidhi kwa wakati; lazima tuwashirikishe wadau wa PETS ili taarifa zao
ziwe ni moja ya misingi ya ufuatiliaji kwa halmashauri," alisema Mhe.
Senyamule.
Pamoja na yote Mhe. Senyamule aliomba CCT kuongeza idadi ya kata
wanazofanyia kazi kutoka 11 hadi zote 34 zilizopo kwa sasa.
Mkuu
wa Wilaya ya Same, Rosemary Senyamule (wa nne toka kushoto) akiwa
katika picha ya pamoja na viongozi wa serikali, dini na wasimamizi wa
mpango wa "Public Expenditure Tracking System" (PETS) waliohudhuria
semina iliyofanyika Same kwa kuwezeshwa na Jumuiya ya Kikristo Tanzania
(CCT).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...