WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe ameagiza taasisi zote zinazohusika na udhibiti wa maudhui ya luninga nchini kubuni mkakati wa pamoja wa kuboresha udhibiti.

Dk Mwakyembe ametoa rai hiyo baada ya kuzikutanisha taasisi hizo za udhibiti leo jijini Dar Es Salaam.

"Nyinyi nyote ni taasisi za Serikali, hivyo tengenezeni mkakati wa kufanya kazi kwa pamoja kudhibiti maudhui mabovu ili kulinda  maadili ya jamii yetu," alisema.Waziri Mwakyembe alifanya mkutano wa pamoja na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Bodi ya Filamu Tanzania (TFB) na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA)."Kuna hitaji za kuongeza uwezo wa kufuatilia maudhui ya luninga ikiwa ni pamoja na filamu zote ili kubaini maudhui hasi kwa jamii yetu na kuzishughulikia ipasavyo kabla hazijaleta madhara kwa jamii," alisema.

Alisema changamoto za ongezeko la mahitaji ya jamii zinazidi kukua kwa haraka kutokana na kasi ya maendeleo hivyo ni vizuri kuhakikisha  kuwa majawabu yake yanapatikana.Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi Susan Mlawi, alisema Wizara itaangalia jinsi ya kuunganisha majukumu ya taasisi zinazosimamia maudhui ya vyombo vya utangazaji nchini ili kuimarisha udhibiti wa pamoja. 

Akiongea katika mkutano wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dodoma mapema wiki hii, Rais John Pombe Magufuli aliiagiza Wizara ya Habari na TCRA kutosita kuvichukulia hatua vyombo vya utangazaji zinavyokiuka kanuni za utangazaji nchini.
 Dk Mwakyembe akizungumza na Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya TCRA,Bi.Valerie Msoka,
 Kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi Suzan Mlawi, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Eng James Kilaba na Mkurugenzi wa Utangazaji wa TCRA, Chief Fredrick Ntobi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...