Na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW
Naibu
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt.
Faustine Ndugulile amezindua programu ya Kikundi Mlezi yenye lengo la
kuwawezesha wanawake wajasilimali wasio katika Sekta rasmi kuleana
wenyewe katika kuanzisha na kuendeleza mitaji na biashara zao.
Dkt.
Ndugulile amezindua programu hiyo wakati alipofanya ziara Wilayani
Kisarawe mkoani Pwani katika zoezi la kuamsha ari ya wananchi
kujishughulisha katika shughuli za maendeleo katika maeneo yao.
Dkt.Ndugulile
amesema kuwa ili kufanikisha kufikia Tanzania ya viwanda Serikali
itaendelea kuwasaidia wajasiliamali wadogo wadogo hasa wanawake katika
kuwawezesha kuanzisha vikundi vitakayoanzisha viwanda vidogo vidogo na
vya kati.
Ameongeza
kuwa lengo la kuzindua Programu ya Kikundi Mlezi ni inalenga
kuwawezesha wanawake wasio katika Sekta rasmi kwa kuwashirikisha
wanawake wajasilimali waliokomaa katika biashara kuwalea na kuwasaidia
wanawake wajasiliamali wanaoanza shughuli hizo.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile akizungumza na vikundi vya wanawake wajasiliamali wa Wilaya ya Kisarawe na maeneo jirani wakati wa uzinduzi wa Programu ya Kikundi Mlezi.
Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi.Sihaba Nkinga akieleza jinsi programu ya Kikundi Mlezi itakavyowasaidia wanawake kuleana na kusaidiana katika biashara zao ili kujikwamua kiuchumi wakati wa uzinduzi wa programu hiyo wilayani Kisarawe.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile akikata utepe kuzindua rasmi Programu ya kikundi Mlezi itakayowezesha wanawake kusaidiana na kuleana wenyewe kwa wenyewe katika kuanzisha biashara ili kujikwamua kiuchumi.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile akionesha kibao kinachoonesha kuzinduliwa rasmi Programu ya kikundi Mlezi itakayowezesha wanawake kusaidia na kuleana wenyewe kwa wenyewe katika kuanzisha biashara ili kujikwamua kiuchumi.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Wizara, viongozi wa Mkoa wa Pwani, Wilaya ya Kisarawe na wanawake wajasiliamali kutoka Wilaya ya Kisarawe mara baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi mkoani hapo. Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...