Katibu Tawala wa Wilaya ya Chemba Ndugu Nyakia Ally Chirukile akichangia damu baada ya kushiriki zoezi la Usafi wa kila jumamosi ya mwisho wa Mwezi,zoezi ambalo lilikwenda sambamba na upandaji wa miti zaidi ya 2000 pembezoni mwa barabara ya Dodoma -Babati kuanzia Kidoka mpaka  Kilema.

Akizungumza baada ya shughuli nzima,Ndugu Nyakia aliwaomba wananchi wa wilaya ya Chemba na mkoa wa Dodoma kwa ujumla,kuunga mkono juhudi za Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mama Samia Suluhu Hassani katika suala zima la uhamasishaji wa kupanda miti na kuhakikisha mkoa huo unakuwa wa kijani .
Baada ya kufanyika shughuli ya uchangiaji Damu,pia kulifanyika tukio la usafi na upandaji wa miti zaidi ya 2000 pembezoni mwa barabara ya Dodoma -Babati kuanzia Kidoka mpaka  Kilema,kuhakikisha mkoa wa Dodoma unakuwa wa kijani,kufuatia kampeni maalum ya upandaji miti iliozinduliwa hivi karibuni na Makamu wa Rais,Mama Samia Suluhu Hassan mkoani humo na kushirikisha viongozi mbalimbali wa Kitaifa na Wadau wengine wa Mazingira.


  Katibu Tawala wa Wilaya ya Chemba Ndugu Nyakia Ally Chirukile akishiriki shughuli ya  upandaji wa miti zaidi ya 2000 pembezoni mwa barabara ya Dodoma -Babati kuanzia Kidoka mpaka  Kilema,baada ya zoezi hio Ndugu Nyakia pia alishiriki tukio la Usafi na uchangiaji wa Damu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...