Mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa wiki ya nenda kwa usalama barabarani Mkoani hapo, iliyozinduliwa na kufanyika viwanja vya Mailmoja, Kibaha.
Kaimu kamanda wa kikosi cha usalama barabarani Mkoani Pwani, Salum Morimori akizungumza wakati wa uzinduzi wa wiki ya nenda kwa usalama barabarani Mkoani hapo, iliyofanyika viwanja vya Mailmoja, Kibaha. (picha na Mwamvua Mwinyi)

Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

MKUU wa mkoa wa Pwani,mhandisi Evarist Ndikilo, amewaasa baadhi ya madereva kuacha kujiingiza kwenye biashara ya usafiri wa vyombo vya moto ikiwemo bodaboda bila kwenda kwenye mafunzo ya udereva na kupata leseni kwani kwa kufanya hivyo ni kuvunja sheria za usalama barabarani. Amesema wapo baadhi ya madereva wanaoendesha vyombo hivyo kwa kujifunza kwa wenzao kwa masaa kisha kuingia barabarani suala ambalo ni kuhatarisha maisha ya abiria wanaowabeba.

Akizindua wiki ya nenda kwa usalama barabarani mkoani humo katika viwanja vya Mailmoja, mhandisi Ndikilo alisema ajali nyingi husababishwa na makosa ya kibinadamu. Alisema kati ya makosa hayo ni pamoja na yanayosababishwa kwa makusudi na madereva hao ikiwemo kuendesha huku wakiwa hawana leseni. Mhandisi Ndikilo alieleza kuwa, pia kuendesha wakiwa wametumia vileo ,kupishana pasipo tahadhali (overtaking),uchovu wa kuendesha masafa marefu na kuendesha vyombo vibovu.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...