Mkuu
wa Wilaya ya Kongwa Mh Deo Ndejembi Leo amefanya Kikao na Waratibu
Elimu Kata 22 wa Wilaya ya Kongwa na idara nzima ya Elimu. Lengo la
Kikao hicho ni kufanya tathimini ya maandalizi ya kupokea wanafunzi
wapya wa darasa la kwanza na kidato cha kwanza kwa mwaka 2018.
Katika mambo yaliyojadiliwa ni pamoja na upungufu wa madarasa,madawati na changamoto nyingine mbalimbali.Pia kuweka mikakati ya kuondoa changamoto hizo ifikapo muda wa usajili.
Katika kikao hicho Mh. Ndejembi alimuagiza Mkurugenzi kuwasimamisha kazi waratibu wawili wa Kata ya Njoge na Lenjulu ili kupisha uchunguzi juu ya tuhuma zao mbalimbali zinazopelekea kutowajibika vema katika vituo vyao vya kazi.
Mkuu wa Wilaya aliwaasa waratibu hao kuachana na kufanya kazi kwa mazoea (business as usual), na kuendana na Kasi ya Serikali ya awamu ya tano kwani Mh Rais amewawekea mazingira mazuri ya kazi ikiwemo posho kwa kila MEK Tsh 450,000/= kila mwezi pamoja usafiri. Hivyo wahakikishe wanatoa huduma bora kwa wananchi.
DC Ndejembi alieleza kuwa kwa mwaka ujao wa 2018 wanatarajia kusajili wanafunzi wapya wengi sana wa Shule za Msingi na Kidato cha Kwanza kwani Sera ya utoaji Elimu Bure imeamsha Morali zaidi kwa Wazazi kupeleka watoto Shule.
Katika mambo yaliyojadiliwa ni pamoja na upungufu wa madarasa,madawati na changamoto nyingine mbalimbali.Pia kuweka mikakati ya kuondoa changamoto hizo ifikapo muda wa usajili.
Katika kikao hicho Mh. Ndejembi alimuagiza Mkurugenzi kuwasimamisha kazi waratibu wawili wa Kata ya Njoge na Lenjulu ili kupisha uchunguzi juu ya tuhuma zao mbalimbali zinazopelekea kutowajibika vema katika vituo vyao vya kazi.
Mkuu wa Wilaya aliwaasa waratibu hao kuachana na kufanya kazi kwa mazoea (business as usual), na kuendana na Kasi ya Serikali ya awamu ya tano kwani Mh Rais amewawekea mazingira mazuri ya kazi ikiwemo posho kwa kila MEK Tsh 450,000/= kila mwezi pamoja usafiri. Hivyo wahakikishe wanatoa huduma bora kwa wananchi.
DC Ndejembi alieleza kuwa kwa mwaka ujao wa 2018 wanatarajia kusajili wanafunzi wapya wengi sana wa Shule za Msingi na Kidato cha Kwanza kwani Sera ya utoaji Elimu Bure imeamsha Morali zaidi kwa Wazazi kupeleka watoto Shule.
Mkuu
wa Wilaya ya Kongwa Mh Deo Ndejembi akizungumza kwenye Kikao na Waratibu
Elimu Kata 22 wa Wilaya ya Kongwa na idara nzima ya Elimu, Lengo la
Kikao hicho ni kufanya tathimini ya maandalizi ya kupokea wanafunzi
wapya wa darasa la kwanza na kidato cha kwanza kwa mwaka 2018.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...