Mkurugenzi
wa Kampuni ya Msama Action Mart, Alex Msama amshukuru Rais Dkt. John
Pombe Magufuli kwa kitendo cha kutoa msamaha kwa wanamuziki maarufu
nchini, Papii Nguza (Papii Kocha) na baba yake mzazi, Nguza Viking (Babu
Seya) aliyekuwa akitumikia kifungo cha maisha katika gereza la Keko
jijini Dar es Salaam.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaama, Msama ambaye ni alikuwa
ni mjumbe wa Bodi wa BASATA na mpigania haki zawasanii na vile vile ni
mlezi wa wasanii mbali mbali amesema jambo alilolifanya ni jema sana na
ametekeleza maagizo ya Mungu ambayo anatushauri tusamehe.
"Ukisoma
hata kwenye vitabu vya biblia suala la kusamehe alishalisema, katika
Mathayo 18:21-22... Ndipo Petro akamjia Yesu na kumwuliza, “Bwana, ndugu
yangu anikosee mara ngapi nami nimsamehe? Je, hata mara saba?” Yesu
akamjibu, ''Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.'
alisema Msama.
Msama
aliongeza kuwa jambo hilo ni kubwa na halina kipingamizi chochote maana
kila kona ya Tanzania maamuzi hayo yamepokelewa kwa mikono miwili.
Aliongeza kuwa wafanyabiashara wote wanaofanya kazi za sanaa ni vyema
wakafuata taratibu kwa kuuza kazi halali zilizo na stika za TRA ambazo
zitawanufaisha wasanii na serikali kwa ujumla.
Hata hivyo, zoezi laukamataji Kazi feki za sanaa litaendelea katika Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni zoezi la nchi nzima.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...