Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
NAIBU Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditye, ametoa siku 14 kuhakikisha bomba la mafuta la Kimataifa linalosambaza mafuta (TIPPER), liwe limeunganishwa kwenye mfumo unaodhibitiwa na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) ili serikali iweze kupata mapato sahihi.
Kutokana na bomba la tipper kuunganishwa katika bandari kumesababisha serikali kupata mapato kwa kampuni hiyo kujisimamia yenyewe.
Akizungumza katika ziara ya kikazi aliyoifanya bandarini hapo jana, Nditye amesema, TPA kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na EWURA wafanye uchunguzi wa haraka kufahamu upotevu wa mapato ya serikali yaliyotokana na Tipper kujiunganishia mafuta kutoka kwenye meli bila kupitia katika kituo cha Kurasini Oil Jet (KOJ).
Amesema Tipper wamekiuka maagizo ya Waziri Mkuu, Kassim Majaaliwa yaliyolewa Februari mwaka jana ya kutaka waunganishe bomba lao katika mfumo wa TPA ili kufahamu kiwango cha mafuta wanayoyachukua.
" Wizi wa waziwazi tangu Februari mwaka jana alipoagiza Waziri Mkuu hadi leo TIPPER mmeshindwa kuunganisha bomba lenu hali inayochangia mapato ya Serikali kuzidi kupotea," alisema Nditye.
Amesema TIPPER waliagizwa na waziri ndani ya mwezi.mmoja wawe wamejiunga katika.mfumo huo lakini cha ajabu maaagizo yamekiukwa hali inayoashiria bado kuna ujanja unaendelea.
Amesema haiwezekani TIPPER wakajiunganisha wenyewe halafu wakajisimamia wao.kufahamu kiwango cha mafuta ya dizeli na ya kula wanayotumia.
Aliagiza pia TPA iimarishe ulinzi kwa mtoa taarifa za upotevu wa mafuta hayo na endapo atapata madhara Serikali.itachukua hatua.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano-Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditye akizungumza na Menejimenti ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) katika ziara yake alipotembelea mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Nchini (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko akitoa taarifa za utendaji wa mamlaka hiyo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano-Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye (Kushoto) wakati Naibu Waziri huyo alipotembelea mamlaka ya Bandari jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano-Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye akizungumza katika ujenzi wa scanner ya ukaguzi katika bandari ya Dar es Salaam.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...