Na Fredy Mgunda,Iringa.
Mbunge wa viti maalam mkoa
wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati amefanya ziara kwenye baadhi ya shule za msingi za
manispaa ya Iringa kwa lengo la kubaini changamoto zilizopo na kuanza
kuzitafutia ufumbuzi kwa lengo la kuboresha mazingira ya wanafunzi kusomea.
Akizungumza mara baada ya
kumaliza zira hiyo ya wiki moja Kabati alisema kuwa amefanya ziara katika shule
ya msingi Kihesa,Igereke,Mtwira na shule ya Kibwabwa na kubaini changamoto
nyingi ambazo anaanza kuzitafutia ufumbuzi hivi karibuni.
“Nimejionea mwenyewe changamoto
zilizopo na naona kama changamoto kwa asilimia kubwa zinafanana hivyo ni kazi
yangu kuanza kutafuta njia ya kuanza kuzitatua changamoto hizo”alisema Kabati.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...