Taswira ya daraja la Mtera, ambalo pia hutumika kama milango ya kupitishia maji ya kusukuma mashine za kufua umeme. picha hii imepigwa Desemba 20, 2017.


NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Mtera


UHARIBIFU wa mazingira unaotokana na mabadiliko ya tabia nchi na shughuli za kibinadamu kwenye bwawa la Mtera sio tu unaathiri kiasi cha maji kwa matumizi ya Kituo cha kufua umeme cha Mtera bali pia unaathiri pakubwa kituo kingine cha kufua umeme cha Kidatu mkoani Morogoro, Mtaalamu wa Mazingira wa Shirika la Umeme nchini TANESCO, Bw. Yusuf Kamote amewaambia waandishi wa habari waliotembelea Kituo cha Kufua Umeme wa Maji cha Mtera, kilichoiko mpakani mwa mikoa ya Dodoma na Iringa.

Ukiachilia mbali mabadiliko ya tabia nchi, shughuli za kibinadamu kandokando ya mito, kunachafua mazingira ya mito hiyo na kupunguza kiasi cha maji na hivyo kuathiri uzalishaji umeme wa maji.

“Tatizo hili ni kubwa watu wanaingilia mito hii, kuna wakulima na wafugaji wanathiri sana, shughuli za kilimo na ufugaji zinaleta mchanga mwingi kwenye maji na hivyo kupunguza kina cha mto na maji yenyewe tunaita siltation, na hiyo ikitokea ujio wa maji kwenye mitambo unapungua na hivyo uzalishaji unapungua kama hivi sasa mnavyoona maji yamepungua.” Alisema.

Bw. Kamote aliwaasa wananchi kuacha kuaharibu mazingira kwani athari zake ni kubwa katika kuendesha mitambo ya kufua umeme ambao ni muhimu kwa uchumi wanchi.“Yawezekana wanafanya shughuli hizo kwa kutokujua athari zake katika uzalishaji umeme, kwa hivyo tunashauri wananchi waelewe kwamba hilo ni tatizo na waache.” Alisetoa rai Bw. Kamote.
Mtaalamu wa Mazingira wa Shirika la Umeme nchini TANESCO, Bw. Yusuf Kamote, akielezea jinsi mabadiliko ya tabia nchi na shughuli za kibinadamu zinavyoathiri bwawa la Mtera. Kushoto ni Mhandisi Myumbilwa
Daraja la Mtera, ambako pia ndiko iliko milango ya kupitishia maji ya kufua umeme
Kaimu Meneja wa Kituo cha kuzalisha umeme wa maji Mtera, Mhandisi David Myumbilwa, akielezea jinsi mashine za kufua umeme zinavyotegemea maji.
Wahariri wakiangalia jinsi moja kati ya mashine mbili za kufua umeme wa maji inavyofanya kazi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...