Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega amewataka maafisa maendeleo kutembelea vijijini ili kuhamasisha maendeleo katika kaya za vijiji kutokana baadhi vijiji kuwa nyuma kimaendeleo.

Kutofika kwa watendaji kuhamasisha maendeleo kunasababisha wananchi kuona serikali haifanyi kazi. Amesema kuwa vijiji vikiwezeshwa vitaleta maendeleo kwa haraka kwani serikali ya awamu ya tano inaitaji kusonga mbele bila kumwacha mwananchi yeyote nyuma katika ukuaji wa uchumi.

Akizungumza katika kijiji cha nyangunguti na Mkenge Kata ya Beta wilayani Mkurunga ,amesema maofisa wa maendeleo wanatakiwa kukimbizana na kasi ya maendeleo kwani muda wa kukaa ofisini umekwisha.

Amesema ili kuimarisha serikali na kumsaidia Rais Dk.John Pombe Magufuli ,watendaji wawe chachu ya maendeo kwa kuwafikia wananchi moja kwa moja. Kwa upade wa wananchi wa kijiji cha Nyangunguti wamemuomba Naibu Waziri huyo kuendelea kuhamasisha maendeleo ili vijiji vikue kwa kasi

Katika ziara ya Vijiji hivyo ameahidi kutoa Mifuko 130 ya saruji ,Mifuko 100 ikiwa ni sehemu ya kuchangia ujenzi wa shule mpya na 30 katika kijiji cha Mkenge kwa ajili sakafu ya shule ya kijiji hicho. Aidha ametoa fedha tasilimu sh.100000 kwa ajili wanafunzi yatima wa kijiji cha Nyangunguti.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa Nyangunguti.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akisalimina na mmoja wa watoa huduma mara baada ya kuwasili katika Zahanati ya kijiji cha Mkenge Mkoa wa Pwani.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akionesha karatasi namna ya udanganyifu wa Korosho unaosababisha soko la zao hilo kuwa na tatizo.
Sehemu ya wananchi wakimsikiliza Naibu Waziri Ulega .Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...