Ntegenjwa Hosseah, Mpwapwa.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa amesema vituo vyote 211 vinavyoongezewa miundombinu ya Afya vinahitaji wataalam wa kutoa Dawa za Usingizi ili kukidhi mahitaji ya wagonjwa watakaofikishwa katika chumba cha Upasuaji pamoja na Wodi ya Kinamama.

Waziri Jafo ameyasema hayo wakati wa ziara yake ya Kikazi Wilayani Mpwapwa na kukagua miradi ya maendeleo iliyompelekea kufika katika ujenzi wa miundombinu ya Afya inayojengwa katika Kituo cha Afya Mima.

Akiwa kituoni hapo alisema ameridhishwa na ujenzi wa miundombinu hiyo ambapo hii ya awamu ya kwanza itakamilika mapema Mwezi Januari 2018 lakini anaona uhitaji wa wataalam wa kutoa Dawa za Usingizi ambao watatoa huduma hizo wakati wa upasuaji na huduma nyingine muhimu.

“Nataka vituo hivi vinapokamilika vianze kufanya kazi mara moja na sio zianze sababu mara wataalamu Fulani hakuna hiki bado sitapenda kusikia hayo ni vyema kwa sasa kila Mkurugenzi wa halmashauri ahakikishe anabainisha wataalam angalau wawili ambao watakwenda kupata mafunzo mafupi ya utoaji wa Dawa hiyo ya Usingizi wakati wa Upasuji”.

Mpaka sasa nimeridhishwa kabisa na kasi ya Ujenzi wa vituo hivi vya Afya na kwa sababu vifaa Tiba pia tunapata kutoka Bohari Kuu ya Dawa sasa kwa pamoja tuangalie maeneo mengine ambayo yataenda sambamba na utoaji wa huduma katika vituo hivi kama wataalamu hawa ambao kwa Takwimu zilizopo kwa sasa bado ni wachache na baada ya ukamilishwaji wa vituo hivi Uhitaji Utakua Mkubwa zaidi alisema Waziri Jafo.

Awali akitoa Taarifa ya Ujenzi Mkurugenzi wa Kampuni ya Global Space East Africa iliyopewa Kazi ya Kujenga Kituo cha Afya Mima Gaston Francis amesema kampuni hiyo hujenga kwa kutumia Teknolojia ya Kisasa iitwayo “Pre-Fabricated Material” ambayo ni nafuu zaidi na ina ubora wa hali ya juu hivyo kwa gharama hiyo ya Mil 500 watajengwa majengo saba huku yakiwa na thamani zote zinazohitajika “Full furnished”.

Aina hii ya Teknolojia hutumika sana maeneo yenye vimbunga, upepo Mkali na Dhoruba mbalimbali na kwa sababu eneo hili la Mima linaathiriwa sana na wadudu Material hii tunayotumia itaenda kuwa suluhisho la kudumu la wadudu hao kwa sababu hawataweza kuathiri hata eneo moja na majengo tutakayojenga na ubora wa material hizi tunazotumia zinadumu kwa Zaidi ya miaka sabini alisema Francis.

Awali katika ziara yake Waziri Jafo alianza kwa kutembelea ujenzi wa barabara ya Lami ( Km 1 ) iliyojengwa kuanza NMB Mpwapwa mpaka Stendi ya Mpwapwa, kukagua Mradi wa Maji Mima pamoja na kuzungumza na wananchi wa Mima kwenye Mkutano wa hadhara.
Mbunge wa Mpwapwa Mhe. George Malima Lubeleje(kushoto) akielezea Umuhimu wa miradi ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa hivi katika sasa kwa Waziri wa Nchi, OR-TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo (kushoto) akimskiliza Mkurugenzi wa Kampuni ya Global Space East Africa Gaston Francis(Kulia) namna wanavyojengwa kwa kutumia Teknolojia ya “Pre Fabricated Material’.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo(kushoto) akikabidhiwa kitendea kazi ili aweze kushiriki kwenye Ujenzi wa Kituo cha Afya kwa kutumia Teknolojia ya “Pre Fabricated Material”.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo(aliyeinama) akishiriki kukata chuma kitakachotumika katika ujenzi wa jengo la Maabara kwa kutumia Teknolojia ya “Pre Fabricated Material”.
Hili ni moja ya Jengo lililojengwa katika Kituo cha Afya Mima kwa Kutumia Teknolojia ya “Pre Fabricated Material” linalojengwa na Kampuni ya Global Space East Africa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...