WANAFUNZI 28 wamehitimu shahada za uzamili Utawala wa Biashara na Biashara Kimataifa katika chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM).
Naibu Mkuu wa Chuo cha Taaluma , Utafiti na Ushauri, Dk. Imanuel Mzava amesema shahada ya uzamili wa Utawala wa Biashara na Biashara Kimataifa inatolewa kwa ushirikiano wa Taasisi ya Biashara ya Kimataifa ya nchini India (Indian Institute of Foreign Trade)
Amesema kuwa shahada hiyo ilinza kutolewa mwaka 2000 na hadi kufikia leo, wanafunzi 600 wamehitimu katika kozi hiyo na wameendelea kupokea wanafunzi wengine wengi.
Mzava amesema kuwa kuanzishwa kwa shahada hiyo nchini kwa ushirikiano wa Taasisi ya India kumewapunguzia gharama wahitaji wa shahada hiyo ambapo walitakiwa wakasome nchini India lakini elimu hiyo hapa hapa nchini kupitia Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM). Pichani juu ni baadhi ya wanafunzi hao wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kulamba nondozz zao, leo katika chuo cha IFM jijini Dar es salaam.
Mdau Alimwene ambaye pia ni mfanyabiashara akiwa na wahitimu wenzake kabla ya kulamba nondozz hizo.
Mdau Alimwenye akilamba Nondozz yako na hapa akikabidhiwa na Naibu Mkuu wa Chuo cha Taaluma , Utafiti na Ushauri, Dk. Imanuel Mzava.
Dada Levina Kato wa Mamlaka ya Bandari pia alikuwa ni mmoja wa waliolamba nondozz.
Mary Massawe pia kutoka Bandari
Mdau Morgard Lumbanga.
Mdau Shaban Omary akipokea Nondozz yake kutoka kwa Naibu Mkuu wa Chuo cha Taaluma , Utafiti na Ushauri, Dk. Imanuel Mzava.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Mdau Shaban Omary akipokea Nondozz yake kutoka kwa Naibu Mkuu wa Chuo cha Taaluma , Utafiti na Ushauri, Dk. Imanuel Mzava.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...