Mwenyekiti wa Makampuni ya Lawrance Sikutwa & Associates (LSA) Bwana Lawrance Sikutwa akizungumza na wafanyakazi wa Kampuni Bima ya Mgen Tanzania Insurance Limited katika hafla ya kufunga mwaka iliyowashirikisha wateja na baadhi ya mawakala wa kampuni hiyo hapa nchini ili kufurahi pamoja, Hafla hiyo imefanyika jana katika makao makuu ya kampuni hiyo Masaki jijini Dar es salaam .
Mwenyekiti wa Makampuni ya Lawrance Sikutwa & Associates (LSA) Bwana Lawrance Sikutwa akifurahia jambo mara baada ya kumkabidhi zawadi Hope Kaiza liyefanya kazi kwenye kampuni ya Mgen Tanzania kwa miaka 10 kwa mafanikio makubwa kushoto ni Mkurugenzi wa Mgen Tanzania Insurance Limited Bw. David Tuhoye .
Mwenyekiti wa Makampuni ya Lawrance Sikutwa & Associates (LSA) Bwana Lawrance Sikutwa akifurahia jambo mara baada ya kuwakabidhi zawadi Mkurugenzi Mtendaji wa Lumumba Insurance Brokers Limited Bw. Jamal Lardhi kushoto na Tiraib Maghembe Mkuu wa Idara ya Fedha Lumumba Insurance Brokers Limited katikati anayewapongeza ni Mkurugenzi wa Mgen Tanzania Insurance Limited Bw. David Tuhoye
Mwenyekiti wa Makampuni ya Lawrance Sikutwa & Associates (LSA) Bwana Lawrance Sikutwa akimkabidhi zawadi Bw. Sudi Simba Afisa Mtendaji Mkuu wa Zurich Group Ltd kwa ushirikiano wa kampuni hiyo kwa Mgen Tanzania Insurance katikati ni Mkurugenzi wa Mgen Tanzania Insurance Limited Bw. David Tuhoye
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...