Na David John

BAADHI ya wananchi wa Kigamboni Gezaulole Kata ya Somangila mtaa wa Mwela jijini Dar es Salaam, wameiomba serikali kulipa fidia kwa wananchi hao ambao walitakiwa kupisha ujenzi shiriki wa mpango Mji.

Wamesema kuwa ni muda mrefu sasa umepita hawajuwi mstakabali wa fidia hiyo nakudai ni vema serikali ikafanya haraka kuwafidia ili waondokane na hali ngumu wanazokutana nazo.

Akizungumza kwaniaba ya wezake mmoja wa waathirika na mchakato huo Marando Nyanda alisema wakati wanaambiwa wapishe tayari wao walikuwa na mazao mbalimbali ambapo Serikali walisema watafidia.

"Sisi kwa kutambua umuhimu wa mradi huu tulikubaliana na Serikali kwamba wangetufidia lakini cha ajabu hadi kufikia leo sisi baadhi ya wakazi wa maeneo haya hatujalipwa. "amesema Marando

Ameongeza kuwa mchakato huo ulikuwa shirikishi lakini hadi kufikia leo watu zaidi ya 160 hawajuwi mstakabali wa malipo yap na kudai nimiaka mitano imepita sasa.

Wananchi hao amesema hakuna asijuwa juu ya jambo hilo kuazia mkuu wa mkoa hadi mawaziri wenye dhamana wanajuwa huku wakimtaka Rais Magufuli kuingilia kati suala hilo ili wao wapate haki zao.

Akizungumzia jambo hilo Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula alisema kuhusu jambo hilo wananchi hao wanatakiwa waende katika ofisi za halmashauri ya kigamboni.

Alisema kuwa kuhusu uboreshaji wa mpango mji katika halmashauri hiyo upo chini ya halmashauri hiyo ya kigamboni hivyo nivema wakafika huko au kuonana na Mkuu wa wilaya hiyo ili kupata ufumbuzi wa jambo hilo.
 
Marando nyanda mmoja wa wakazi wa Kigamboni Gazaulole ambaye anasotea fidia ya kupisha ujenzi shirikishi wa mpango mji katika eneo hilo picha na David John.  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...