Na Agness Francis, Blogu ya Jamii
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dr. Harrison Mwakyembe   amezungumza  na wasanii wa tasnia mbalimbali hapa nchini akiwataka kuendeleza  na kuutangaza uzalendo wetu unaoendana na maadili yetu, ikiwa kauli mbiu ni nchi yangu kwanza.
Waziri huyo amesema hayo  jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa uwanja wa taifa  akiwahimiza Wasanii hao ambao ni kioo cha jamii kuwa na  mchango mkubwa  katika kuijenga nchi yetu. "Waandishi wa habari pia ni miongoni mwa mashujaa wetu waliotufikisha hapa tulipo" amesema waziri Mwakyembe.
Aidha Waziri  Mwakyembe  asema kuwa siku ya Ijumaa 8, Desemba mwaka huu  Dodoma kutakuwa na uzinduzi rasmi wa kampeni ya uzalendo kwanza kwa nchi yangu ambapo uzinduzi huo  utahudhuruwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwa ni mzalendo wa kwanza katika ujenzi wa taifa letu
 Naibu waziri wa habari sanaa utamaduni na michezo Juliana Shonza  amesikitishwa na baadhi ya wasanii ambao ni vioo vya jamii hapa nchini kutokuwa na maadili ya kizalendo kwa kutumia vibaya vyombo vya mawasiliano  kwa kupiga picha zisizofaa na kutuma kwenye mitandao ya kijamii,Na amewataka kuwa  mabalozi wazuri katika  kutangaza uzalendo kwanza Hapa nchini
Hata hivyo naibu  huyo  ametoa pongezi za dhati kwa  Mrisho mpoto akiwa mzalendo alietoa wazo hilo na wasanii wenzake, Na amesema kuwa  wizara imeipa uzito kampeni hii na kuamua kuwa inde mkoani kwaajili ya uzinduzi huo.
Vile vile pia naibu Shoza  amempongeza mwanamashumbwi Ibrahim class kwa kuwa mzalendo kwa kuwa bingwa wa 3 barani Afrika na   asie na mpinzani  nchini Tanzania na kumkabidhi hundi ya shilingi milioni 18 laki 2 na 40 elfu
Nae bondia Ibrahimu class  amemalizia kwa kusema kuwa mazoezi na kujiamini ndio kinachomfanya afanye vizuri katika mashindano yake ya ndani na  nnje ya nchi na ametoa shukrani zake za dhati kwa watanzaia kwa kumuunga mkono katika mapambano yake.

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dr. Harrison Mwakyembe akizungumza na wageni waalikwa katika mkutano huo kuhusu uzinduzi wa uzalendo kwanza utakaofanyika tarehe 8, Desemba mwaka huu mkoani Dodoma.
Naibu waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza  akizungumza na wageni waalikwa kuhusu uvunjifu wa maadili ya kizalendo unaofanywa na baadhi ya wasanii hapa nchi Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa  uwanja wa Taifa.
Naibu waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza  akimkabidhi bondia Ibrahimu Class  hundi ya shilingi milioni 18,240,000 na kumpa pongezi kwa kuweza kutetea ubingwa wake.
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dr. Harrison Mwakyembe  akimpa pongezi  mwanamasumbwi wa Tanzania Ibrahim Class kwa kazi nzuri anayoifanya na kuwa mzalendo hapa nchini.
Mwanamasumbwi  Ibrahim Class akizungumza na wageni waalikwa kuhusu mafanikio yake katika mashindano yake kwa ujumla na kuwapongeza watanzania kwa kumuunga mkomo.

Wasanii mbalimbali  hapa nchini waliojitokeza katika kuhudhuria mkutano huo  leo Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa  uwanja wa taifa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...