KIPA wa Timu ya Jamuhiri Ali Khamis akijaribu kuokoa mpira uliopigwa na Mshambuliaji wa Timu ya Azam Benard Arthur akifunga bao la kwanza kwa Timu yake katika dakika ya 26 ya mchezo huo uliofanyika katika Uwanja wa Amaan Zanzibar . Timu ya Azam imeshinda mchezo huo kwa bao 4. -0 dhidi ya Timu ya Jamuhuri katika michuano ya Kombe la Mapinduzi , doli la PIli la Timu ya Azam limefungwa na mshambuali Salmin Hoza katika dakika ya 48 ya mchezo huo kipindi cha pili na Bao la Tatu la Azam limefungwa na katika dakika ya 56 ya mchezo huo kupitiamchezaji wake Yahya Zayd.Timu ya Azam imefunga mchezo huo kwa kuandika bao la nne kupitia mshambuliaji wake Peter Paul katika dakika ya 79 ya mchezo huo uliofanyika katika uwanja wa amaan Zanzibar.
WACHEZAJI wa Timu ya Azam wakishangilia bao lao la ushindi la nne lililofungwa na mshambuliaji wake Peter Paul katika kipindi cha pili cha mchezo huo.
BEKI wa Timu ya Jamuhuri Abdallah Juma akijaribu kumzuiya mshambuliaji wa Timu ya Azam wakati wa mchezo wao wa Kombe la Mapinduzi mchezo uliofanyika Uwanja wa Amaan Zanzibar Timu ya Azam imeshinda bao 4 -0.
MSHAMBULIAJI wa Timu ya Azam Bruce Kangwa akiruka kiunzi cha Beki wa Timu ya Jamuhuri Abdullatif Omar, wakati wa mchezo wao wa Kombe la Mapinduzi uliofanyika Uwanja wa Amaan Timu ya Azam. imeshinda bao 4 -0.
KIPA wa Timu ya Jamuhuri Ali Khamis akidaka mpira huku mshambuliaji wa Timu ya Azam Benard Arthur akiwa tayari kutowa mashambulizi wakati wa mchezo wao wa Kombe la Mapinduzi uliofanyika Uwanja wa Amaan Zanzibar Timu ya Azam imeshinda bao 4 -0.
BEKI wa Timu ya Jamuhuri Yussuf Makame akiokoa mpira golini kwao huku mshambuliaji wa Timu ya Azam Bruce Kangwa akijiandaa kuchukua mpira huo, wakati wa michuano ya Kombe la Mapinduzi mchezo uliofanyika Uwanja wa Amaan Zanzibar Timu ya Azam imeshinda bao 4 -0/uul wa tayari kul .(Picha na Othman Maulid)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...