Basi la kampuni ya Tahmeed lenye namba za usajili T483 BFL limeungua moto katika Kijiji cha Kabuku wilayani Handeni. 

Kwamujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoani Tanga, SACP Edward Bukombe alisema basi hilo ambalo lilikuwa na abiria 9 tu kutoka Dar es salam liliungua moto kutokana na hitilafu za umeme. 

Alisema Dereva wa bus hilo Bakari Said (34) alihisi halipo vizuri katika mfumo wa engine akasimamisha gari kisha kuwaomba abiria washuke.

Hata hivyo hakukuwa na mtu aliyejeruhiwa kutokana na ajali hiyo. Hii ni mara ya pili kwa basi la kampuni hiyo kupata hitilafu Kwenye mfumo wa injini na kuungua moto.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...