Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ofisi ya Zanzibar inashiriki kwa mara nyingine tena Tamasha la Nne la Biashara linaloendelea viwanja vya Maisara mjini Unguja Zanzibar kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 54 ya Mapinduzi Zanzibar.

Miongoni mwa huduma ambazo Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa inatoa kwenye Banda la Maonesho ni kutoa elimu kuhusu Vitambulisho, Kutoa taarifa za Usajili kwa Wananchi ambao wamesajiliwa na hawajapata Vitambulisho vyao, kuanisha matumizi ya Vitambulisho na huduma ya Usajili kwa wageni (foreigners)

Usajili Vitambulisho vya Taifa kwa Tanzania Zanzibar umekamilika kwa asilimia 99.7 na kwa wale wananchi ambao hawajasajiliwa Usajili unaendelea kwenye Ofisi za Wilaya zilizonguliwa kwenye kila Wilaya Unguja na Pemba.



Wafanyakazi wa NIDA ofisi ya Zanzibar pamoja na Kaimu Mkurugenzi Ofisi ya NIDA Zanzibar (Mwenye Kaunda) wakiwa katika Banda la maonyesho katika viwanja vya Maisara
Wafanya kazi wa NIDA wakijiandaa kumpokea mgeni rasmi kwenye banda lao lililopo viwanja vya Maisara Zanzibar.
 
Wafanyakazi wa NIDA wakiwahudumia wananchi waliofika katika banda la maonyesho katika viwanja vya Maisara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...