Pamoja na zoezi la Usajili linalohusisha ujazwaji wa fomu za maombi pamoja na kuchukuliwa alama za Kibaiologia pamoja na Picha, Mkoa wa Songwe umeanza zoezi msingi la Mapingamizi ambapo wananchi wanapata fursa ya kuhakiki taarifa zao pamoja na kuweka mapingamizi kwa mtu yoyote wanayehisi si raia au si Mkazi wa eneo husika na amefanya udsajili wa maombi ya Kitambulisho cha Taifa, ambapo Bi. Coletha amewasihi Wananchi wa katanganyifu kusajiliwa Vitambulisho vya Taifa.

Zoezi hili lililoanza sambamba na kuendelea kwa usajili kwa Kata ambazo hazijakamilisha linahusisha Kata za ichenjezya, vwawa na mlowo Wilayani Mbozi mkoani Songwe baada ya kukamilisha hatua ya awali ya usajili.

Kwa mujibu wa Afisa Usajili Wilaya ya Mbozi Bi. Bi. Coletha Peter amesema zoezi hilo litahusisha wananchi wote wa mkoa wa Songwe na kuwataka kujitokeza kwa wingi kwenye mbao za matangazo ambako picha zote za waombaji wa Vitambulisho vya Taifa zimebandikwa pamoja na majina yao.

Amesema kama Mamlaka wamejipanga kuhakikisha wanapokea mapingamizi ya watu wote watakao bainishwa kwa njia ya wazi na siri na kuhakikisha Mamlaka inayafanyia kazi majina hayo mapema sambamba na kuanza uchakataji wa taarifa za waombaji wote waliokamilisha taratibu za Usajili ili vitambulisho vianze kutolewa kwa wakati.
Afisa Usajili Mamlaka ya Vitambilsho vya Taifa akichukua alama za Vidole vya mmoja wa wananchi wa Kijiji cha Mbonji waliofika Katika moja ya Vituo vya Usajili ili kupatiwa huduma ya usajili na Utambuzi.
Wananchi wa Kata ya Itaka Kijiji cha Itaka wengi wao wakiwa ni akina Mama, wakijificha Mvua nje ya moja ya Kituo cha Usajili wakati wakishiriki zoezi la Usajili Vitambulisho vya Taifa linaloendelea kwenye Kata hiyo
Wananchi wakiendelea na zoezi la kuchambua fomu nje ya Kituo cha Usajili katika kijiji cha Nsani Kata ya Itaka Wilaya ya Mbozi kabla ya kwenda kupatiwa huduma ya Usajili na Utambuzi uliohusisha uchukuaji wa alama za kibaiologia, saini ya kielektroniki pamoja na Picha.
Wananchi wa Kijiji cha Mbonji kata ya Itaka Wilaya ya Mbozi wakiwa katika foleni kuelekea kupata huduma ya usajili na utambuzi zoezi linaloendela katika kata nzima ya Itaka.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...