WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi,
Luhaga Mpina ameamuru kufanyika ukaguzi mpya wa hesabu za fedha kwenye
masoko yote ya kimataifa ya samaki na mazao yake yaliyoko katika Ziwa
Victoria ili kuhakiki uhalali wa mapato ya Serikali yaliyokusanywa
katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.
Masoko hayo yatakayohusika na ukaguzi huo ni pamoja na Kirumba Mwanza, Nyakalilo Buchosa Mwanza ,Kasenda Chato Geita, Magalini Muleba Kagera, Kemondo Bukoba Kagera na Mwigobero Musoma Mara ambapo wafanyabiashara watakaobainika walihusika kufanya udanganyifu wa mapato watatakiwa kurejesha fedha hizo walizoiibia Serikali kwa kipindi hicho ambapo Watumishi wa Umma nao waliohusika kuhujumu mapato hayo watasakwa popote walipo na kufikishwa kwenye vyombo vya dola kukabiliana na mashtaka ya kuhujumu wa rasimali za nchi .
Hatua hiyo ya Waziri Mpina imekuja kufuatia kubaini kuwepo udanganyifu mkubwa katika biashara ya samaki, dagaa,mabondo, na mapanki akibainisha kuwepo tabia ya kupunguza uzito na idadi ya magunia,kubadilisha matumizi ya vibali,kuchanganya mizigo ya ndani na nje ya nchi kwenye malori, kuanzishwa kwa masoko ya kimataifa yasiyo rasmi na wafanyabiashara wakubwa wa mazao ya uvuvi kutolipa kodi za mapato kutoka TRA.
Pia Waziri Mpina ameamuru kufutwa kwa masoko yote yasiyo rasmi yaliyopewa hadhi ya kimataifa ikiwemo soko la Nyakalilo na Magalini ambapo amemuagiza Katibu Mkuu Uvuvi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Yohana Budeba kuwaondoa na kuwapangia vituo vingine vya kazi watumishi waliokuwepo kwenye masoko hayo.
Mkuu wa Wilaya ya Chato Shabani Ntarambe (aliyesimama) akimweleza jambo Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina(mwenye kofia) wakati wa mkutano wa hadhara kwenye soko la kimataifa la samaki la Kasenda wilayani Chato leo, ambapo Waziri ameamuru kufanyika ukaguzi mpya wa hesabu za fedha kwenye masoko yote ya kimataifa ya samaki na mazao yake yaliyoko katika Ziwa Victoria ili kuhakiki uhalali wa mapato ya Serikali yaliyokusanywa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.Kulia ni Diwani wa kata ya Kasenda Muganza Mwita.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina(mwenye kofia katikati) akiwa kwenye moja ya boti inayotumika kwa Uvuvi wa samaki kwenye soko la kimataifa la samaki la Kasenda wilayani Chato leo, Kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chato Bathromeo Christiani, Kushoto ni Diwani wa kata ya Kasenda Muganza Mwita. (Picha na John Mapepele)
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina(mwenye kofia) akiwahutubia wananchi kwenye soko la kimataifa la samaki la Kasenda wilayani Chato leo, ameamuru kufanyika ukaguzi mpya wa hesabu za fedha kwenye masoko yote ya kimataifa ya samaki na mazao yake yaliyoko katika Ziwa Victoria ili kuhakiki uhalali wa mapato ya Serikali yaliyokusanywa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. (Picha na John Mapepele)
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina(mwenye kofia) akikagua ofisi za soko la kimataifa la samaki la Kasenda wilayani Chato leo, Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Uvuvi bi Mwanaidi Mlolwa. Nyumba niYohana Mikumbe Mtekinolojia wa samaki katika soko la Kasenda. . (Picha na John Mapepele)
Umati wa wananchi waliohudhuria mkutano wa Waziri Luhaga Mpina kwenye soko la kimataifa la samaki la Kasenda wilayani Chato leo, ameamuru kufanyika ukaguzi mpya wa hesabu za fedha kwenye masoko yote ya kimataifa ya samaki na mazao yake yaliyoko katika Ziwa Victoria ili kuhakiki uhalali wa mapato ya Serikali yaliyokusanywa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. (Picha na John Mapepele)
Masoko hayo yatakayohusika na ukaguzi huo ni pamoja na Kirumba Mwanza, Nyakalilo Buchosa Mwanza ,Kasenda Chato Geita, Magalini Muleba Kagera, Kemondo Bukoba Kagera na Mwigobero Musoma Mara ambapo wafanyabiashara watakaobainika walihusika kufanya udanganyifu wa mapato watatakiwa kurejesha fedha hizo walizoiibia Serikali kwa kipindi hicho ambapo Watumishi wa Umma nao waliohusika kuhujumu mapato hayo watasakwa popote walipo na kufikishwa kwenye vyombo vya dola kukabiliana na mashtaka ya kuhujumu wa rasimali za nchi .
Hatua hiyo ya Waziri Mpina imekuja kufuatia kubaini kuwepo udanganyifu mkubwa katika biashara ya samaki, dagaa,mabondo, na mapanki akibainisha kuwepo tabia ya kupunguza uzito na idadi ya magunia,kubadilisha matumizi ya vibali,kuchanganya mizigo ya ndani na nje ya nchi kwenye malori, kuanzishwa kwa masoko ya kimataifa yasiyo rasmi na wafanyabiashara wakubwa wa mazao ya uvuvi kutolipa kodi za mapato kutoka TRA.
Pia Waziri Mpina ameamuru kufutwa kwa masoko yote yasiyo rasmi yaliyopewa hadhi ya kimataifa ikiwemo soko la Nyakalilo na Magalini ambapo amemuagiza Katibu Mkuu Uvuvi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Yohana Budeba kuwaondoa na kuwapangia vituo vingine vya kazi watumishi waliokuwepo kwenye masoko hayo.

Mkuu wa Wilaya ya Chato Shabani Ntarambe (aliyesimama) akimweleza jambo Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina(mwenye kofia) wakati wa mkutano wa hadhara kwenye soko la kimataifa la samaki la Kasenda wilayani Chato leo, ambapo Waziri ameamuru kufanyika ukaguzi mpya wa hesabu za fedha kwenye masoko yote ya kimataifa ya samaki na mazao yake yaliyoko katika Ziwa Victoria ili kuhakiki uhalali wa mapato ya Serikali yaliyokusanywa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.Kulia ni Diwani wa kata ya Kasenda Muganza Mwita.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina(mwenye kofia katikati) akiwa kwenye moja ya boti inayotumika kwa Uvuvi wa samaki kwenye soko la kimataifa la samaki la Kasenda wilayani Chato leo, Kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chato Bathromeo Christiani, Kushoto ni Diwani wa kata ya Kasenda Muganza Mwita. (Picha na John Mapepele)

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina(mwenye kofia) akiwahutubia wananchi kwenye soko la kimataifa la samaki la Kasenda wilayani Chato leo, ameamuru kufanyika ukaguzi mpya wa hesabu za fedha kwenye masoko yote ya kimataifa ya samaki na mazao yake yaliyoko katika Ziwa Victoria ili kuhakiki uhalali wa mapato ya Serikali yaliyokusanywa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. (Picha na John Mapepele)

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina(mwenye kofia) akikagua ofisi za soko la kimataifa la samaki la Kasenda wilayani Chato leo, Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Uvuvi bi Mwanaidi Mlolwa. Nyumba niYohana Mikumbe Mtekinolojia wa samaki katika soko la Kasenda. . (Picha na John Mapepele)

Umati wa wananchi waliohudhuria mkutano wa Waziri Luhaga Mpina kwenye soko la kimataifa la samaki la Kasenda wilayani Chato leo, ameamuru kufanyika ukaguzi mpya wa hesabu za fedha kwenye masoko yote ya kimataifa ya samaki na mazao yake yaliyoko katika Ziwa Victoria ili kuhakiki uhalali wa mapato ya Serikali yaliyokusanywa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. (Picha na John Mapepele)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...