Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi akionesha sehemu   ya Udongo ambao umechanganyika na takataka zilizokuwa chini ya barabara ya Msasani CCBRT ,ambayo imekuwa ikimeguka kila siku kutokana na mkandarasi wa awali  aliojenga barabara hiyo kuipitisha juu ya udongo wenye takataka na kusababishia hasara kwa serikali kila Mwaka.DC Hapi alieleza kuwa ujenzi  huo wa awali umeiingiza Serikali Hasara kutokana na baadhi ya watendaji wa Serikali kula rushwa na kufumbia macho ujenzi huo wa barabara juu ya dampo. 
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi akiwaonya wakazi wa Tandale kwa Tumbo juu ya utupaji taka hovyo katika mitaro ya Maji iliyopo pembezoni mwa barabara,kama ionekanavyo pichani ikiwa imejaa maji taka na kuhatarisha afya za wakazi wa eneo hilo.
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi akionesha barabara ya Magomeni Kondoa inayokarabatiwa na Wakala wa Barabara nchini Tarura  mara baada ya kuwa na Mashimo mengi na kufanya kushindwa kupitika
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi akichota sehemu ya udongo uliokuwa ukisumbua barabara ya Msasani CCBRT ambao ulikuwa umechanganyika na Taka.
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi akikagua barabara ya kuelekea Sleepway Masaki Jijini Dar es Salaam ambayo imeharibika na Mashimo Makubwa na sasa inakarabatiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...