Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) imefanya mnada wa hadhara wa kuuza meno ya viboko vipande 12,467 yenye uzito wa kilo 3,580.29 katika ofisi zake ndogo katika Jengo la Mpingo, jijini Dar es Salaam ambapo jumla ya makampuni 19 yenye leseni daraja la kwanza yameshiriki katika mnada huo.
Mnada huo umefanyika chini ya usimamizi wa Wizara ya Fedha na Mipango ambapo kampuni ya On Tours Tanzania Limited imeibuka mshindi kwa kwa kununua meno hayo kwa jumla ya shilingi 30,900,000/=
Awali akizungumza katika mnada huo, Mwenyekiti kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Karerema Kwaleh aliwataka wafanyabiashara kuzingatia masharti mnada huo.
Ambapo Karerema alimtaka mfanyabiashara yeyote atakeibuka mshindi kulipia asilimia ishirini na tano (25%) ya bei papo hapo na asilimia sabini na tano (75%) italipwa yote katika muda wa siku kumi na nne (14) baada ya mnada.
Kufuatia sharti hilo baada ya kutangazwa kwa mshindi, Mwakilishi kutoka Kampuni hiyo, Grey Kilas aliweza kulipia asilimia kiasi hicho cha asilimia ishirini na tano (25%) papo hapo na asilimia sabini na tano (75%) atailipia ifikapo Februari 11, 2018.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...