Na  Bashir  Yakub.

Haki ya  kusajili  na  kuwa  na  chama  cha  siasa  ipo  kwa kila  mtanzania.  Hata  wewe  unaweza  kuwa  na  chama  cha  siasa  ikiwa  utataka  kufanya  hivyo.  Wako  wanaofikiri  kusajili  chama  siasa  ni  jambo  kubwa  mno. Laa  hasha  ni  jambo  la  kawaida    na  utaratibu  wa  usajili  si  mgumu  kama  wengi  wanavyodhani.

Tutaona  hapa  utaratibu  wa  kusajili  chama  cha  siasa.  Sheria  namba  5 ya  1992  Sheria ya  Vyama  vya  Siasa  na  kanuni  zake  za  mwaka  1992 ndizo  zinazoeleza  utaratibu utakaoelezwa  hapa  chini.

USAJILI  HUPITIA  HATUA  KUU  MBILI.

Kwa  mujibu  wa  kifungu  cha8( 1 ) cha  sheria  ya  vyama  vya  siasa  usajili  hupitia  katika  hatua  kuu  mbili.
Kwanza  usajili  wa  muda  na  pili  usajili  wa  kudumu.  Kwahiyo  ili  usajili  chama  cha  siasa  yakupasa  kupitia  hatua  hizi  mbili.

1.      USAJILI  WA  MUDA(PROVISIONAL REGISTRATION).      
  
Usajili  wa  muda  umeelezwa  katika kifungu  cha  9  cha  sheria  hiyo.  Usajili  wa  muda  maana  yake  chama  kitasajiliwa   na  kitaruhusiwa  kufanya  baadhi  ya  kazi  ila  usajili  huo  utakuwa  haujakamilika  mpaka  baada  ya  kutimiza  masharti, sifa  na  viwango  vilivyowekwa  na  sheria   ndani  ya  muda  maalum  ulioainishwa na sheria.  Usajili wa muda ndio  unaoanza  na  utaratibu  wake  ni huu ;
( a ) Andaa  katiba  ya  chama na  hakikisha  unakuwa  nayo. Mnajua  kila  chama  cha  siasa  huwa  na  katiba  yake, basi  hiyo  ndiyo  inayotakiwa hapa.
( b ) Hakikisha  mko  waanzilishi  wasiopungua  wawili.
( c ) Andaa  kanuni  za  chama. Kanuni  na  katiba  ni  tofauti. Kanuni  ndizo  zinazotafsiri  katiba kwahiyo  kanuni  hutokana  na  katiba.


                    KUSOMA  ZAIDI sheriayakub.blogspot.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...