- Mkandarasi asiyeanza kazi ifikapo Machi 2 kukiona cha moto
- Viongozi TANESCO, REA wawasilishe taarifa kila robo mwaka

Na Veronica Simba – Dodoma.

Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amekutana na watendaji mbalimbali wanaosimamia na wanaotekeleza miradi ya awamu ya tatu ya kusambaza umeme vijijini na kutoa maagizo mazito yanayolenga kufanikisha mradi huo kikamilifu.

Mkutano huo uliofanyika mwishoni mwa Juma, Januari 13 mwaka huu, Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma, ulihudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu.
Akizungumza katika mkutano huo, Waziri Kalemani alitoa maagizo kwa wajumbe ambao ni wazalishaji na wasambazaji wa nguzo, transfoma na nyaya za umeme, wakandarasi wanaotekeleza mradi husika katika maeneo mbalimbali nchini na wataalam wanaosimamia utekelezaji wa mradi huo kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Wakala wa Nishati Vijijini (REA); kuhakikisha kila mmoja anatimiza wajibu wake ipasavyo.
Kwa upande wa wakandarasi, Dkt. Kalemani aliwaagiza kuhakikisha kila mmoja anaanza utekelezaji wa kazi halisi (physical work) kabla ya tarehe 2 Machi mwaka huu vinginevyo Serikali itawachukulia hatua za kisheria. “Asiwepo mkandarasi yeyote ambaye atakuwa hajaanza kazi baada ya tarehe hiyo, alisisitiza.”
 Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (katikati) akisisitiza jambo wakati akiongoza kikao baina yake na wadau mbalimbali wanaotekeleza miradi ya usambazaji umeme vijijini awamu ya tatu. Kushoto ni Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu na kulia ni Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara, Haji Janabi.
 Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (aliyesimama) akizungumza wakati wa Mkutano na wadau mbalimbali wanaotekeleza miradi ya usambazaji umeme vijijini awamu ya tatu. Kushoto kwake ni Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani.
 Wakandarasi mbalimbali wanaotekeleza miradi ya usambazaji umeme vijijini awamu ya tatu, wakielezea hatua waliyofikia katika utekelezaji wake katika kikao baina yao na Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani, Dodoma mwishoni mwa Juma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...