Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni Mstaafu George Mkuchika (kushoto) akiwasili chuo cha Chuo Cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) Tawi la Mtwara ikiwa ni mwendelezo wa ziara zake za kutembelea matawi ya chuo hicho nchini kulia ni Mkurugenzi wa TPSC Tawi la Mtwara Dkt. Emmanuel Shindika,ziara hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni Mstaafu George Mkuchika (katikati) akipata maelezo kutoka Mkurugenzi wa TPSC Tawi la Mtwara Dkt. Emmanuel Shindika (kushoto) akiwa katika moja ya madarasa ya chuo hicho tawi la Mtwara ikiwa ni mwendelezo wa ziara zake za kutembelea matawi ya chuo hicho nchini, ziara hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki.Wengine pichani ni watumishi wa chuo hicho.
Kwaya ya TPSC tawi la Mtwara ikitoa burudani mbele ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni Mstaafu George Mkuchika (Hayupo pichani), aliyefanya ziara fupi chuoni mwishoni mwa wiki sambamba na kupokea taarifa ya tawi na kusikiliza changamoto za watumishi na wanachuo.
Baadhi ya wanachuo wa Chuo cha Utumishi wa Umma TPSC tawi la Mtwara, wakimsikiliza kwa makini waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni Mstaafu George Mkuchika (Hayupo pichani), aliyefanya ziara fupi chuoni hapo mwishoni mwa wiki sambamba na kupokea taarifa ya chuo na kusikiliza changamoto za watumishi na wanachuo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...