*Ataka takwimu za kahawa ziwe tayari ifikapo Feb. 28
WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri za Mji na
Wilaya za Mbinga wahakikishe kuwa wanaunda kanda za kilimo na
kuwasambaza maafisa kilimo wao badala ya kuwaacha wakae maofisini.
Ametoa
agizo hilo jana jioni (Ijumaa, Januari 5, 2018) wakati akizungumza na
watumishi na madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga pamoja na
Halmashauri ya Mji wa Mbinga, kwenye ukumbi wa Jumba la Maendeleo, mjini
Mbinga.
“Mkurugenzi
wa TC na DC chuja maafisa kilimo ulionao na uhakikishe wanabakia watatu
tu. Abaki DALDO, mtu wa horticulture na mthamini, wengine wote
wasambaze kwenye kanda ili wasimamie wakulima wakiwa huko huko. Hili
litekelezwe na Mkuu wa Wilaya ulisimamie” alisema.
Aliwataka
maafisa kilimo wa zao la kahawa waende vijijini na kufanya sensa ili
waweze kubaini wana wakulima wangapi wanaozalisha kahawa. “Afisa kilimo
wa wilaya lazima ujue kijiji kina wakulima wangapi wa kahawa, na wana
ekari ngapi? Na katika ekari hizo, ana miche mingapi? Hii itaisaidia
Serikali ijue inahitaji dawa za aina gani, mbolea kiasi gani na miche
mingapi kwa wakulima wake,” alisema.
“Ninataka hizi takwimu ziwe zimekamilika ifikapo tarehe 28 Februari, mwaka huu,” alisisitiza.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiangalia mche wa Kahawa, wakati alipotembelea kituo cha utafifti wa zao la kahawa (TACRI) kilichopo kwenye kijiji cha Ugano Wilaya ya Songea, Mkoani Ruvuma, akiwa kwenye ziara ya kikazi ya siku tano Mkoani Ruvuma, kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Kituo hicho, Dkt. Deusdedit Kilambo. Januari 5, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua kitalu cha miche ya Kahawa, wakati alipotembelea kituo cha utafifti wa zao la kahawa (TACRI) kilichopo kwenye kijiji cha Ugano Wilaya ya Songea, Mkoani Ruvuma, akiwa kwenye ziara ya kikazi ya siku tano Mkoani Ruvuma, kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Kituo hicho, Dkt. Deusdedit Kilambo na katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme Januari 5, 2018
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiangalia kahawa kwenye mashine ya kusagia kahawa, wakati alipotembelea kiwanda cha kahawa cha Mbinga Coffee kilichopo Mbinga Mjini Wilayani Songea, Mkoani Ruvuma, kushoto ni Meneja Uzalishaji Rabiel Ulomi na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Christina Mndeme. Januari 5, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiangalia sampuli za kahawa kwenye, wakati alipotembelea kiwanda cha kahawa cha Mbinga Coffee kilichopo Mbinga Mjini Wilayani Songea, Mkoani Ruvuma, kulia ni Meneja Uzalishaji Rabiel. Januari 5, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongea na Watumishi wa Halmashauri ya Mbinga, Mkoani Ruvuma, akiwa kwenye ziara ya kikazi ya siku tano Mkoani Ruvuma. Januari 5, 2018.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...