Na Shamimu Nyaki-WHUSM
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe ameunda kamati ya watu kumi na moja watakaopitia Katiba ya kusimamia mchezo wa ngumi  za kulipwa hapa nchini pamoja na kukusanya maoni  namna bora ya kuendesha mchezo huo itakayoanza kazi  kuanzia Januari 03 hadi 31 ambapo  itakuwa chini ya Baraza la Michezo la Taifa (BMT) .

 Akizungumza na wadau wa mchezo huo Jijini Dar es Salaam Mhe.Waziri ameiagiza Kamati hiyo kufanya kazi kwa pamoja katika kuunda mfumo mpya utakaolinda maslahi ya mabondia na wahusika wote wa mchezo huo ili kuleta heshima ya mchezo huo hapa nchini.

“Naomba mshirikiane katika kazi hii vunjeni makundi yenu ili mfanye kazi kwa maslahi ya Taifa na wanamasumbwi wetu,mkifanya hivyo tutaleta hamasa kubwa kwa watu wengi kujiunga na mchezo huu ambao unaleta ajira kwa vijana wetu”.Alisema Mhe.Waziri Mwakyembe.

 Kamati hiyo itaongozwa na mwenyekiti Emmanueli Salehe ambaye ni mdau mkubwa wa ngumi hapa nchini,akisaidiwa na makamu Mwenyekiti Joe Enea ambaye ni Mwalimu wa ngumi pamoja na katibu Bw.Yahya Pori ambae pia ni mdau wa mchezo huo.
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza leo Jijini Dar es Salaam na Wadau wa mchezo wa ngumi hapa nchini ambapo ameunda Kamati ya Watu kumi na moja watakaoandaa Katiba ya mchezo huo ndani ya mwezi huu. 
 Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo nchini Bw. Yusuph Singo(aliyesimama) akizungumza leo Jijini Dar es Salaam na Wadau wa mchezo wa ngumi hapa nchini  kabla ya Mhe Waziri Mwakyembe wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo kuuunda Kamati ya Watu kumi na moja watakaoandaa Katiba ya mchezo huo ndani ya mwezi huu.
 Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Bw. Mohamedi Kiganja akitoa muongozo wa kikao  baina ya Mhe.Waziri  Harrison Mwakyembe (aliyekaa katikati) na wadau wa ngumi nchini leo Jijini Dar es Salaam.
 Mwanamasumbwi wa zamani Bw.Yassin Ustadhi akichangia mawazo wakati wa kikao cha Mhe. Waziri Mwakyembe wa Wizara ya Habari  Utamaduni Sanaa na Michezo na wadau wa mchezo wa ngumi leo Jijini Dar es Salaam.
Picha ya pamoja

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...