Na Shamimu Nyaki-WHUSM
Waziri
wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe ameunda
kamati ya watu kumi na moja watakaopitia Katiba ya kusimamia mchezo wa
ngumi za kulipwa hapa nchini pamoja na kukusanya maoni namna bora ya
kuendesha mchezo huo itakayoanza kazi kuanzia Januari 03 hadi 31
ambapo itakuwa chini ya Baraza la Michezo la Taifa (BMT) .
Akizungumza
na wadau wa mchezo huo Jijini Dar es Salaam Mhe.Waziri ameiagiza Kamati
hiyo kufanya kazi kwa pamoja katika kuunda mfumo mpya utakaolinda
maslahi ya mabondia na wahusika wote wa mchezo huo ili kuleta heshima ya
mchezo huo hapa nchini.
“Naomba
mshirikiane katika kazi hii vunjeni makundi yenu ili mfanye kazi kwa
maslahi ya Taifa na wanamasumbwi wetu,mkifanya hivyo tutaleta hamasa
kubwa kwa watu wengi kujiunga na mchezo huu ambao unaleta ajira kwa
vijana wetu”.Alisema Mhe.Waziri Mwakyembe.
Kamati
hiyo itaongozwa na mwenyekiti Emmanueli Salehe ambaye ni mdau mkubwa wa
ngumi hapa nchini,akisaidiwa na makamu Mwenyekiti Joe Enea ambaye ni
Mwalimu wa ngumi pamoja na katibu Bw.Yahya Pori ambae pia ni mdau wa
mchezo huo.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza leo Jijini Dar es Salaam na Wadau wa mchezo wa ngumi hapa nchini ambapo ameunda Kamati ya Watu kumi na moja watakaoandaa Katiba ya mchezo huo ndani ya mwezi huu.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo nchini Bw. Yusuph Singo(aliyesimama) akizungumza leo Jijini Dar es Salaam na Wadau wa mchezo wa ngumi hapa nchini kabla ya Mhe Waziri Mwakyembe wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo kuuunda Kamati ya Watu kumi na moja watakaoandaa Katiba ya mchezo huo ndani ya mwezi huu.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Bw. Mohamedi Kiganja akitoa muongozo wa kikao baina ya Mhe.Waziri Harrison Mwakyembe (aliyekaa katikati) na wadau wa ngumi nchini leo Jijini Dar es Salaam.
Mwanamasumbwi wa zamani Bw.Yassin Ustadhi akichangia mawazo wakati wa kikao cha Mhe. Waziri Mwakyembe wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo na wadau wa mchezo wa ngumi leo Jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...