Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

KIKOSI cha Yanga kesho kinatarajia kukwea pipa alfajiri na mapema ili kuwahi mechi yao  dhidi ya Ihefu ikiwa ni mchezo wa kombe la Azam Sports HD  utakaopigwa kwenye Uwanja wa Sokoine  Jijini Mbeya majira ya saa 10 jioni siku hiyo hiyo.

Timu ya Ihefu inayoshiriki ligi darala la pili ilifanikiwa kuwaondoa timu ya Mbeya City katika mchezo wao wa kwanza huku Yanga wakiwaondoka timu ya Reha na kufanikiwa kuingia hatua ya pili ya kombe la Shirikisho FA .

Yanga itakayoshuka dimbani kesho kuvaana na Ihefu, kikosi chao kinatarajiwab kuondoka alfajiri ya kesho ili kuwahi mchezo utakaochezwa majira ya saa 10 alasiri huku wakilalamikia ratiba kutokuwa rafiki kwa upande wao.

Akizungumza na Globu ya Jamii, Meneja wa timu ya Yanga amesema kuwa kikosi kitaondoka na wachezaji wao wote isipokuwa wale waliokuwa majeruhi ambapo bado hawajaungana na wenzao kikamilifu.

"wachezaji watakaokosekana katika mchezo wa kesho ni saba ambao bado hawajaanza kuungana na wenzao katika mazoezi ya jumla ila wachezaji wengine wote wako katika hali nzuri," amesema Hafidh.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...