Na-Jumbe Ismailly MANYONI  

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wilaya ya Manyoni,Mkoani Singida imemuhukumu Musa Haruna (47) mkazi wa Kijiji cha Mtimkavu,kata ya Itigi,wilayani Manyoni kutumikia adhabu ya mwaka mmoja jela baada ya kumtia hatiani kwa kosa la wizi wa bomba tatu za chuma zenye thamani ya shilingi milioni mbili laki mbili elfu na themanini mali ya Wakala wa barabara Tanzania(TANROADS).
Mahakama hiyo ilimtia hatiani mshitakiwa baada ya kukiri na kukubaliana na hoja zote za mashtaka,ikiewemo kukamatwa na bomba tatu za chuma zilizopatikana kwa njia isiyo halali,kufikishwa polisi na kufikishwa Mahakamani.
Awali Mwendesha Mashtaka wa serikali,Geofrey Luhanga alidai kwamba sept,23,mwaka jana saa 1;30 usiku katika eneo la mtaa wa Majengo,mjini Itigi,Musa Haruna alikutwa na bomba za chuma tatu zenye thamani ya shilingi milioni 2 na laki mbili elfu na themanini zilizopatikana kwa njia isiyo halali mali ya Wakala wa barabara Tanzania (TANROADS).
Aidha Luhanga alidai pia kwamba hakuna kumbukumbu za makosa ya nyuma hivyo aliiomba Mahakama hiyo kwamba adhabu zinazotolewa na Mahakama kwa makosa ya aina hiyo ziwe kali ili ziwe fundisho kwa watu wengine wenye nia ya kutenda kosa kama hilo.
Kwa mujibu wa Mwendesha Mashtaka huyo wa serikali mabomba hayo yalikuwa yakitumika kwa alama mbali mbali za barabarani na makosa hayo yamefanywa kwa makusudi na mshitakiwa huyo na kutokana na kukosekana kwa alama hizo imekuwa vigumu kwa watumiaji barabara kujua maeneo hatarishi kwa kuwa hakuna alama zinazoonyesha tahadhari hizo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...