Na Agness Francis -Globu ya jamii

KAMPUNI ya Simu za mkononi Airtel Tanzania imeamua kuzindua promosheni ya Yatosha Intanenti kwa wale wanaonunua vifurushi vya bando la Yatosha SMATIKA Intanenti.

Akizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi huo,leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Masoka Airtel Tanzania Isack Nchunda, amesema kampuni hiyo imeamua kutoa zawadi kwa wateja wake wanaotumia bando la SMATIKA Intanenti.

Kwani wamekuwa waaminifu kwao na wanaendelea kutoa hamasa ili kuendelea kumtumia huduma zao. Nchunda amesema promosheni hiyo ya Yatosha Intanenti itakuwa ni ya muda wa siku 30, ambapo kutakuwa na droo 3 za kila wiki kati ya siku za Jumatatu, Jumatano na Ijumaa,

"Kwa ndroo ya kila siku wateja 1000 watajishindia bando ya Intanenti yenye 1 Gb kwa kila mmoja, wakati droo kubwa itakuwa na washindi 10,huku 5 wakijishindia simu za Smartphone na wengine 5 kujinyakulia modern,"amesema Nchunda.

Aidha Meneja Uhusiano Airtel Tanzania,Jackson Mmbando amewataka wateja wao kutokuwa na hofu katika mchakato mzima wa uwendeshaji wa promosheni hiyo. "Itakuwa ni promosheni ya wazi sana itasimamiwa na Bodi ya Michezo ya Kubahatisha hapa nchini.Kila mteja atakaeshiriki moja kwa moja ataingia kwenye droo ya bahati na kuambiwa kuwa ameshinda au hajashinda"amesema Mmbando.
 Kushoto Meneja uhusiano Airtel Tanzania Jackson Mmbando na kulia ni Mkurugenzi Masoko Airtel Isack Nchunda  katika zoezi la uzinduzi Wa Promosheni ya SMATIKA Intanenti leo makao makuu ya Airtel Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Masoko Wa Airtel Tanzania Isack Nchunda  akizungumza na waandishi Wa Habari leo katika Makao makuu ya Airtel Jijini Dar es Salaam  kuhusu promosheni hiyo itakavyokuwa ikifanyika ili Kuibuka mshindi Katiba Bahati nasibu hiyo.
Meneja uhusiano Airtel Tanzania Jackson Mmbando akizungumza na waandishi  Wa Habari  leo katika Makao makuu ya Airtel Jijini Dar es salaam kuhusu promosheni  hiyo iliyozinduliwa kama zawadi kwa wateja wake.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...