
“Nimepokea kwa masikitiko
taarifa za kifo cha Mzee Kingunge Ngombale Mwiru, natoa pole kwa familia
ya marehemu na Watanzania kwa ujumla kwa
kumpoteza mwanasiasa Mkongwe katika nchi hii ambaye licha ya kuwahi kuwa Mbunge
lakini pia ameitumikia Serikali katika nyadhifa mbalimbali,” alisema.
“Binafsi
nilifanya kazi kwa karibu na Mzee Kingunge wakati wa Bunge letu na pia kwenye
Bunge la Katiba ambapo tulikuwa wote kamati namba nane nikiwa Mwenyekiti wake,
mchango wake ulitusaidia sana” aliongeza Mheshimiwa Spika.
Mheshimiwa
Spika amemuomba Mwenyezi Mungu awape subira, nguvu na faraja familia, ndugu,
jamaa na marafiki katika kipindi hiki kigumu cha kupotelewa na mpendwa wao.
Imetolewa
na:
Ofisi ya Spika
S.L.P. 941
DODOMA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...