Na Dixon Busagaga, Siha
Chama cha Mapinduzi (CCM) kupitia mgombea wake Dkt Godwin Mollel kimeshinda kiti cha ubunge katika jimbo la Siha baada ya kupata kura 25,611 sawa na asilimia 80 akimshinda mpinzani wake Elvis Mosi (Chadema) aliyepata kura 5,905 sawa na asilimia 18.5.
Chama cha Mapinduzi (CCM) kupitia mgombea wake Dkt Godwin Mollel kimeshinda kiti cha ubunge katika jimbo la Siha baada ya kupata kura 25,611 sawa na asilimia 80 akimshinda mpinzani wake Elvis Mosi (Chadema) aliyepata kura 5,905 sawa na asilimia 18.5.
Akizungumza kabla ya kukabidhi Cheti cha uthibitisho kwa kuchaguliwa kwake,Msimamizi wa Uchaguzi katika jimbo hilo Valerian Juwal amesema mgombea Tumsifueli Mwanry (CUF) amepata kura 274 sawa na asilimia 0.9 huku mgombea wake chama cha Sauti ya Umma (SAU) akipata kura 170 sawa na asilimia 0.6.
Dkt Godwin Mollel akikabidhiwa cheti cha uthibitisho kwa kuchaguliwa kwake na Msimamizi wa Uchaguzi katika jimbo hilo Valerian Juwal
Dkt Godwin Mollel akifurahia pamoja na watu aliombatana kushuhutia tukio hilo
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...