Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akimuapisha kuwa Kamishna wa
Polisi Zanzibar (CP) Mohamed Hassani Haji, leo Makao Makuu ya Jeshi
hilo jijini Dar es salaam, baada ya kuteuliwa na Mheshimiwa Rais na Amiri
Jeshi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli.
Kamishna wa Polisi Zanzibar (CP) Mohamed Hassani Haji, akiweka saini
hati ya kiapo baada ya kuapishwa na Mkuu wa Jeshi hilo IGP Simon Sirro,
Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es salaam, Kamishna Haji aliteuliwa na
Mheshimiwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Dkt. John Magufuli.
Kamishna wa Polisi Zanzibar (CP) Mohamed Hassani Haji, akitoa neno
mbele ya Maofisa Wakuu Waandamizi na askari wa vyeo mbalimbali
(hawapo pichani) baada ya kuapishwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP
Simon Sirro, kuwa kamishna wa Polisi Zanzibar huku akiahidi kufanyakazi
kwa uzalendo na kumsaidia IGP Sirro katika majukumu ya kulinda usalama
wa raia na mali zao.
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, na Kamishna wa Polisi Zanzibar
(CP) Mohamed Hassani Haji, wakiwa katika picha na Maofisa wa Jeshi hilo
baada ya hafla ya kumuapisha kamishna wa Polisi Zanzibar kukamilika leo
Makao Makuu ya jeshi hilo jijini Dar es salaam. Picha na Jeshi la Polisi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...