Na Said Mwishehe, Blogu ya jamii

KADA mpya wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Patrobas Katambi ameeleza sababu zinazochangia kudhoofika kwa vyama vya upinzani nchini.

Amesema kuyumba kwa vyama hivyo kunachangiwa na ubinafsi waviongozi wake ambao wengine wageuza Chama ni mali yao na kutoamaamuzi ambayo si shirikishi.
 
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana,Katambi amesema kuwa tanguameondoka Chadema ambako alikuwa Mwenyekiti wa Vijana na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho amekuwa kimya muda mrefulakini ameona ni vema akasema mambo kadhaa kuhusu hali ya kisiasa nchini.

Kuhusu vyama vya siasa kuyumba, Katambi amesema zipo sababuambazo zimekuwa zikichangia vyama hivyo kushindwa kuwa imara namatokeo yake kubaki kulalamikia kila jambo ambalo linafanywa naSerikali hata liwe lenye maslahi kwa nchi.
 
"Upinzani umeshindwa kujenga chama taasisi kwani hivi sasa kilachama ni cha mtu.vyama vingi ni vya watu na si taasisi.Dhana yataasisi ni kwamba sheria ,kanuni na taratibu lazima zifuatwe"Kama mtu anadharau katiba na misingi iliyowekwa basi huo niudikteta. Wapinzani kabla ya kukimbilia kugombea udiwani na ubunge wajikite kwanza kujenga taasisi, kama wameshindwa kuheshimu katiba za vyama vyao wanapate uhalali wa kudai Katiba,"amesema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...