Na Said Mwishehe, Glogu ya jamii
WABUNGE
kutoka majimbo mbalimbali nchini kupitia Chama ChaMapinduzi (CCM),
wamewaomba wananchi wa jimbo la Kinondoni jijiniDar es Salaam
kuhakikisha Februari 17, mwaka huu wanamchaguamgombea ubunge wa chama
hicho, Abdallah Mtulia katika uchaguzi
mdogo jimboni humo.
Wamesema
Mtulia ndio chaguo sahihi kwa wananchi wa Kinondoni nakwamba akiwa
mbunge watashirikiana naye katika kufanikishachangamoto za wananchi
zinapata ufumbuzi wake.Pia wameeleza namna ambavyo wabunge wa CCM
wamekuwa wamojabungeni katika kupigania maendeleo ya wananchi tofauti na
wabungewa upinzani ambao kila kitu wao ni kupinga hata liwe jambo
lamaendeleo.
Wakizungumza
kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika wanja wa People Kigogo
wilayani Kinondoni jijini, wabunge hao waCCM wamewaomba wananchi
kutofanya makosa kwenye uchaguzi huohuku wakitoa sababu mbalimbali za
kwanini Mtulia anastahili kuwa mbunge wa jimbo hilo.
Mgeni
rasmi kwenye kampeni hizo ambaye pia ni Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein
Bashe (CCM) amewaomba wananchikumchagua Mtulia kwani ndio mgombea
sahihi na wanaamini akiwambunge watashirikiana naye kutatua kero za
wananchi.
"Nimekuja
kuzungumza na ninyi kuwaomba tarehe 17,siku yaJumamosi wote mkamchague
Mtulia, lakini si tu kumchagua lazimatuseme kwanini mumchague
Mtulia.Ndio mgombea mwenye sifa zoteza kuwa mbunge wa Kinondoni,"amesema
Bashe.
Pia
amesema kwenye kampeni hizo wapo wanaotoa hoja kuwa Serikali ya CCM
haitaki mfumo wa vyama vingi, ambapo amefafanua hoja hiyo haina maana
yoyote kwani mwaka 1992 licha ya watanzania wengi kutaka mfumo wa chama
kimoja uendelee lakini uamuzi ulitolewa wa kuingia mfumo vyama vingi.
"Mwaka
1992, watanzania walipata fursa ya kuchagua tuingie kwenye mfumo wa
vyama vingi au laa.Waliotaka vyama vingi walikuwa asilimia 20 na
waliosema chama kimoja kiendelee walikuwa asilimia 80."Mwaka 1995
tukafanya uchaguzi wa vyama vingi na CCM ikashinda, hivyo CCM hatuna
hofu na mfumo wa vyama vingi na ndio maana tumeendelea kushinda katika
kila chaguzi.
"Pia
wapo wanaotoa hoja CCM hakuna demokrasia hili nalo halina ukweli.CCM
demokrasia ipo tena ya kutosha.Ndani ya CCM tunaweza kutofautiana
kimtazamo, tunaweza kutofautiana kwa hoja na wakati mwingine tukashikana
mashati lakini ukweli utabaki tunafanya hayo yote kwasababu ya
demokrasia tuliyonayo,"amesema Bashe.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...