Nteghenjwa Hosseah,Chemba.

Naibu Waziri Ofisi yaRais- TAMISEMI Mhe. Joseph George Kakunda ameiagiz ahalmashauri ya Wilaya ya Chemba kumsimamisha Mhandisi wa Maji wa Halmashauri hiyo kwa kushindwa kusimamia miradi ya maji.

Mhe.Kakunda alitoa maagizo hayo wakati wa ziara yake Wilayani humo aliyoifanya ambapo alikagua miradi ya maji na kuzungumza na wananchi wa vijiji vya Lahoda,Kisande na Honta.

Baada ya kufanya ukaguzi huo na kubaini mapungufu yaliyopo kwenye miradi ya maji sambamba na kumsimamisha Mhandisi wa Maji pia aliagiza OR-TAMISEMI kufanya Ukaguzi wa Kitaalamu (Technical Audit) ya miradi yote ya maji ambayo imeonekana kwa macho kutotekelezwa kwa kiwango na bado haijaanza kufanya kazi katika Halmashauri ya Chemba.

“Serikali imetoa Fedha nyingi sana kwa ajili ya miradi hii ili kupunguza kero kwa wananchi wetu lakini wasimamizi wa Miradi hawatekelezi wajibu wao ipasavyo katika kusimamia miradi hiyo na wananchi wetu bado wananednelea kuteseka kwa sababu ya Uzembe wa watu wacheche hii haitakubalika lazima wachukuliwe hatua” Alisema Kakunda.

Naibu Waziri Kakunda wakati wa ziara hiyo pia alitembelea Shule ya Msingi Lahoda na alikutana na mwananfunzi mwenye ulemavu wa ngozi na kuelekeza Halmashauri ya Chemba iwei na mpatia mahitaji muhimu mwanafunzi huyo.
Naib wa Waziri OR-TAMISEMI Mhe. Joseph Kakunda akikagua mradi wa maji Lahoda-Kisanda wakati wa ziara yake Wilayani Chemba.
Naibu Waziri OR-TAMISEMI Mhe.Joseph kakunda (kulia) akizungumza na mwanafunzi Fatuma Ramadhani wakati alipotembelea shule ya Msingi Lahoda.
NaibU Waziri OR-TAMISEMI Mhe. Joseph Kakunda akikagua mradi wa maji Lahoda-Kisand
NaibU Waziri OR-TAMISEMI Mhe. Joseph Kakunda akizungumza na wananchi wa vijiji vya Lahoda,Kisanda na Honta wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Wilaya ya Chemba.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...