*Waziri Ndalichako asema Taifa limepata pigo kubwa, aomba utulivu
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
SERIKALI
kupitiza Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi imesema
itagharamia mazishi ya mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha
Usafirishaji(NIT) Aqwilina Akwiline ambaye amepoteza maisha baada ya
kupigwa risasi Februari 16 mwaka huu eneo la Mkwajuni jijini Dar es
Salaam
Imesema kifo cha mwanafunzi huyo ni pigo
kubwa kwa familia, Serikali,Wizara ya Elimu,wanafunzi, ndugu,
jamaa na marafiki huku ikiomba Watanzania wote kuwa watulivu katika
kipindi hiki wakati uchunguzi wa kifo hicho ukiendelea kufanywa na
vyombo vya dola.
NI PIGO KWA TAIFA
Akizungumza
Dar es Salaam leo kuhusu kifo cha Aqwilina aliyepigwa risasi akiwa
kwenye daladala, Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa
Joyce Ndalichako amesema Taifa limepata pigo kubwa kwa kuondokewa na
mwanafunzi huyo ambaye hakuwa na hatia ya aina yoyote.
Amesema
kabla ya tukio la kupigwa risasi mwanafunzi huyo alikuwa amebeba barua
kwenda kuomba kufanya mafunzo kwa vitendo lakini kifo kimekatisha ndoto
zake na harakati za kuisaka elimu kwa ajili ya maendeleo ya Taifa letu.
Prof.Ndalichako
amesema tukio la kifo hicho kimegusa hisia za watanzania wengi na Rais
,Dk.John Magufuli mbali ya kutoa pole kwa familia na wananchi wote
ameonesha kuguswa na tukio hilo.
"Ni msiba
mkubwa ambao umelipata Taifa letu kwa kifo cha mwanafunzi wetu
mpendwa.Kifo kimetokea wakati wa kudhibiti maandamano yaliyofanyika
Februari 16 mwaka huu huko Kinondoni.Tunatoa pole kwa familia, ndugu,
jamaa na marafiki pamoja na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji.
"Serikali
imepata pigo kubwa kwani inatumia fedha nyingi kwa ajili ya kuosmesha
wanafunzi wa kitanzania na mwanafunzi aliyefariki ni miongoni mwa
wanafunzi aliyekuwa anasoma kwa mkopo wa Serikali.Mwanafunzi huyu
alikuwa mtiifu na amefariki .Ni msiba ambao hakika umetugusa sisi
wote,"amesema.
SERIKALI KUGHARAMIA MSIBA
Wakati
huo huo, Profesa Ndalichako amesema imeamua kuchukua jukumu la
kugharamia msiba huo hadi pale mwanafunzi huyo atakapopumzishwa kwenye
nyumba yake ya milele wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro.
"Kama
ambavyo nimetangulia kueleza hapo awali namna ambavyo kila mmoja wetu
ameguswa na kifo cha mpendwa wetu lakini Serikali kwa niaba ya Wizara ya
Elimu tumechukua jukumu la kugharamia msiba huu.
"Tunaomba
katika kipindi hiki Watanzania wote tuungane katika kushiriki kwenye
msiba wa mpendwa wetu na nitoe rai kwa wanafunzi wote wakiwamo wa elimu
ya juu kuwa watulivu wakati hatua mbalimbali zikiendelea
kufanyika.Waliohusika wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria,"amesema
Prof. Ndalichako.
Ameomba wananchi wote kuwa
kwa sasa si vema kuanza kulaumiana na badala yake ni kuwa wamoja na
wenye utulivu wa kati mwili wa mwanafunzi huyo ukisubiriwa kupumzishwa na wakati hatua nyingine za vyombo vya dola vikiendelea na uchunguzi wake.
Pichani kati ni Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Prof Joyce Ndalichako akizungumza mbele ya Waandishi wa habari mapema leo mchana jijini Dar,kuhusu kifo cha Mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji(NIT) Aqwilina Akwiline ambaye amepoteza maisha baada ya kupigwa risasi Februari 16 mwaka huu eneo la Mkwajuni -Kinondoni jijini Dar es Salaam,kushoto ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Hamad Masauni pamoja na kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Elimu,Dkt.Akwilapo
Baadhi ya Waandishi wa vyombo vya habari wakiendelea kurekodi na kusikiliza yaliyokuwa yakizungumzwa na viongozi waandamizi wa Serikali kufuatia kifo cha Mwanafunzi huyo,kilichotokea kwa kupiga risasi hivi karibuni Kinondoni,jijini Dar.Picha na Michuzi Jr.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...