Mamlaka ya mapato mkoani Mtwara (TRA) imezifungia hotel tatu mkoani humo pamoja na kituo cha kuuza mafuta kwa kushindwa kulipa kodi ya malimbukizo ya madeni.

Hotel zilizofungiwa ni Naff Beach, Naf blue, BNN pamoja na kituo cha Mnarani Petrol Station ambao kwa pamoja wanadaiwa zaidi ya Shilingi bilioni moja ,ambazo ni malimbukizo ya madeni ya nyuma kwa kipindi cha miaka mitatu.

Afisa mwandamizi wa huduma na elimu kwa mlipa kodi mkoa wa Mtwara, Flavian Byabato amesema zoezi hilo ni endelevu kwa mkoa mzima.

“Ni madeni ambayo yametokana na ukaguzi kwa kipindi cha miaka mitatu nyuma,kikubwa walipe kodi,tunafungia kwa mambo mbalimbali kama malimbikizo ya madeni ya muda mrefu,matumizi sahihi ya mashine za EFD katika kutoa na kudai risiti sahihi inayoakisi gharama halisi ya malipo na kutii sheria za kodi kama kutunza kumbukumbu,”amesema Byabato

Byabato amesema endapo wadaiwa watashindwa kulipa madeni yao watachukua hatua nyigine kama kukamata mali au kuwapeleka mahakamani,kama hawatajitokeza kuomba na kuahidi ni lini watalipa madeni kwani hakuna aliyejitokeza kufanya hivyo.

Aidha amesema pia yapo maduka madogo ambayo yamefungiwa na kwa sasa wako wilayani Masasi wanaendelea na ukaguzi.

Pichani hoteli ya Naff Beach ikiwa imezungushiwa utepe na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...