Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa (kushoto) akizungumza katika kikao cha kubadilishana uzoefu kati ya wajumbe wa nchi ya Lesotho na Tanzania. Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi wa Lesotho, Mhe. Lehlohonolo Moramotse (kulia) ameongoza ujumbe huo uliokuja kwa ziara ya mafunzo nchini Tanzania.
Baadhi ya maofisa waandamizi kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano nchini wakiwa kwenye kikao cha kubadilishana uzoefu kati ya wajumbe wa nchi ya Lesotho na Tanzania.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Eng. Patrick Mfugale akielezea namna TANROADS inavyotekeleza kazi zake kwenye kikao cha kubadilishana uzoefu na wajumbe wa nchi ya Lesotho na Tanzania. Ujumbe huo unaongozwa na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi wa Lesotho, Mhe. Lehlohonolo Moramotse pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi wa Lesotho, Mathabathe Hlalele.
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi wa nchi ya Lesotho, Mathabathe Hlalele (katikati) akizungumza kwenye kikao cha kubadilishana uzoefu kati ya wajumbe wa nchi hiyo na Tanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...