Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akipulizia dawa shamba la pamba wilayani Kwimba. Uzalishaji wa pamba nchini unatarajiwa kuongezeka mara tano msimu huu wa kilimo 2017/2018 kutokana na juhudi mbalimbali zilizofanywa na Bodi ya Pamba kuhamasisha wakulima kuachana na kilimo cha mazoea na kuanza kuzingatia kanuni za kilimo bora cha pamba, kuimarika kwa mfumo wa upatikanaji na usambazaji wa pembejeo, ubora wa mbegu za kupanda zilizosambazwa kwa wakulima na kuongezeka kwa eneo la uzalishaji wa pamba. 

Akiongea katika ziara ya kukagua maendeleo ya uzalishaji wa mbegu bora wilayani Igunga, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Pamba Tanzania Bwana Marco Mtunga amesema, uzalishaji unatarajiwa kuongezeka kwa takriban asilimia 400 kutoka tani 133,000 zilizozalishwa msimu wa 2016/17 hadi kufikia zaidi ya tani 600,000 msimu huu wa 2017/18.

 Aliendelea kueleza kwamba, eneo la uzalishaji wa pamba limeongezeka kutoka ekari 659,000 hadi ekari 3,000,000 ambapo jumla ya tani 26,500 za mbegu zimepandwa zikiwemo tani 8,000 za mbegu za msimu uliopita zilizokuwa kwa wakulima. Kuongezeka kwa eneo la uzalishaji wa pamba kumetokana na uhamasishaji uliofanywa katika maeneo inakolimwa pamba, kuongezeka kwa mikoa mipya ya Dodoma na Katavi katika uzalishaji wa pamba na bei nzuri ya pamba waliyolipwa wakulima msimu uliopita.
Waziri wa Kilimo, Eng. Charles Tizeba, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Pamba, Marco Mtunga na Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri wakiongea na mkulima wa pamba wilayani Igunga. 
Waziri wa Kilimo, Eng. Charles Tizeba na Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Pamba, Marco Mtunga wakikagua zao la pamba wilayani Igunga. 
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella na Mkuu wa Wilaya ya Kwimba, Mtemi Msafiri wakikagua shamba la pamba wilayani Kwimba 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...