Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe akimkaribisha ofisini mgeni wake, Balozi wa Uholanzi nchini, Jeroen Verheul mara baada ya kuwasili. 
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe akiwa kwenye mazungumzo na Balozi wa Uholanzi nchini, Jeroen Verheul. Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe amekutana na Balozi wa Uholanzi nchini, Jeroen Verheul na kufanya nae mazungumzo kuhusu mpango wa kukamilisha mradi wa maji wa kitaifa wa Handeni (HTM) uliopo katika wilaya za Handeni na Korogwe, mkoani Tanga. 

Mazungumzo hayo yaliyofanyika kwenye ofisi za wizara za Ubungo Maji, Jijini Dar es Salaam, yalilenga katika kutatua changamoto za mradi huo ili uweze kukamilika na kutoa huduma kwa ufanisi kwa wakazi ambao kwa sasa wamefikia 300,000 kulinganisha na 180,000 kama lengo la awali katika vijiji 79 vya wilaya za Handeni na Korogwe. 

Katika kikao hicho Waziri Kamwelwe na Balozi Verheul walikubaliana hatua za haraka zichukuliwe kwa lengo la kuondoa vikwazo vyote na kutekeleza mpango huo mara moja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...