Na Said Mwishehe
KWA heshima na taadhima, naomba nitumie nafasi hii kuwasalimia wananchi wa Jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Natoa
salamu zangu kwenu nikitambua kuwa pamoja na shughuli nyingine za
ujenzi wa nchi yetu , pia mpo kwenye kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo
hilo.Sababu za kufanyika za uchaguzi huo unatokana na uamuzi wa
aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF)
Maulid Mtulia kuamua kujiuzulu ubunge.Baada ya kujiuzulu akaondoka CUF
na kujiunga CCM.
Sioni
umuhimu wa kurudia sababu ambazo amezitoa Mtulia wakati anatangaza
kujiondoa CUF.Hata hivyo moja ya sababu amedai alipokuwa CUF alijikuta
akiwa kwenye wakati mgumu kutokana na mpasuko uliopo.Tunafahamu
ndani ya CUF hakuko sawa kutokana na tofauti ya misimamo na mitazamo
baina ya vingozi wa juu wa chama hicho.Hivyo Mtulia akaona bora ajiweke
kando.Ndio sababu ambayo ameitoa.
Pia
akasema
juhudi za Rais ,Dk.John Magufuli za kuleta maendeleo zimemfanya aone
haja ya kuunga mkono kwa kujiunga na CCM.Najua kila mtu anayo nafasi ya
kuchambua na kupima anachosema Mtulia.Kwa sasa Mtulia anagombea tena
ubunge wa Kinondoni kwa tiketi yaCCM.Kampeni zinaendelea Kinondoni na
Mtulia ni miongoni mwa wanaomba kura kwa wananchi.
Katika uchaguzi huo ushindani upo kati ya Mtulia na mgombea ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya Chadema Salimu Mwalimu.Ni
ushindani haswa na kila chama kilipozindua kampeni rasmi walitoa tambo
nyingi.Tunasubiri mwisho wa tambo hizo utakuaje.
Kila
mmoja anaamini ataibuka na ushindi.Chadema wanaamini Kinondoni ni ya
Salumu Mwalimu na hivyo hivyo CCM nao wanaamini Kinondoni ni ya
Mtulia.Sawa
yupo mgombea wa TLP ,Dk.Godfrey Malisa ambaye naye anawania jimbo
hilo.Najua wapiga kura ndio wenye kuamua nani awe mbunge wao baada ya
kila mmoja kupita na kutoa sera za chama chake kuhusu nini watafanya
kwenye jimbo hilo.
KUSOMA ZAIDI MAKALA HII BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...