Na Said Mwishehe
KWA heshima na taadhima, naomba nitumie nafasi hii kuwasalimia wananchi wa Jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Natoa salamu zangu kwenu nikitambua kuwa pamoja na shughuli nyingine za ujenzi wa nchi yetu , pia mpo kwenye kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo hilo.Sababu za kufanyika za uchaguzi huo unatokana na uamuzi wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF) Maulid Mtulia kuamua kujiuzulu ubunge.Baada ya kujiuzulu akaondoka CUF na kujiunga CCM.
Sioni umuhimu wa kurudia sababu ambazo amezitoa Mtulia wakati anatangaza kujiondoa CUF.Hata hivyo moja ya sababu amedai alipokuwa CUF alijikuta akiwa kwenye wakati mgumu kutokana na mpasuko uliopo.Tunafahamu ndani ya CUF hakuko sawa kutokana na tofauti ya misimamo na mitazamo baina ya vingozi wa juu wa chama hicho.Hivyo Mtulia akaona bora ajiweke kando.Ndio sababu ambayo ameitoa.

Pia akasema juhudi za Rais ,Dk.John Magufuli za kuleta maendeleo zimemfanya aone haja ya kuunga mkono kwa kujiunga na CCM.Najua kila mtu anayo nafasi ya kuchambua na kupima anachosema Mtulia.Kwa sasa Mtulia anagombea tena ubunge wa Kinondoni kwa tiketi yaCCM.Kampeni zinaendelea Kinondoni na Mtulia ni miongoni mwa wanaomba kura kwa wananchi.
Katika uchaguzi huo ushindani upo kati ya Mtulia na mgombea ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya Chadema Salimu Mwalimu.Ni ushindani haswa na kila chama kilipozindua kampeni rasmi walitoa tambo nyingi.Tunasubiri mwisho wa tambo hizo utakuaje.
Kila mmoja anaamini ataibuka na ushindi.Chadema wanaamini Kinondoni ni ya Salumu Mwalimu na hivyo hivyo CCM nao wanaamini Kinondoni ni ya Mtulia.Sawa yupo mgombea wa TLP ,Dk.Godfrey Malisa ambaye naye anawania jimbo hilo.Najua wapiga kura ndio wenye kuamua nani awe mbunge wao baada ya kila mmoja kupita na kutoa sera za chama chake kuhusu nini watafanya kwenye jimbo hilo.

KUSOMA ZAIDI MAKALA HII BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...