Na Agness Francis Globu ya jamii 

Kikosi cha YangaSc  Kilichoelekea Nchini Botswana katika mchezo wa marudiano dhidi ya Township Rollers katika michuano  inayoendelea ya Klabu Bingwa Afrika. 

Mchezo huo wa marudiano unatarajiwa kuchezwa kesho machi 17 mwaka huu huko Nchini Botswana. 

Mchezo uliopita ambao  ulichezwa Jijini Dar es Salaam uwanja wa Taifa wawakilishi wa Tanzania katika michuano hiyo walicharazwa mabao 2-1.

Yanga anakabiriwa na kibarua kigumu  ambapo anatakiwa kushinda magoli zaidi ya 2 kwa bila ili kuweza kupata tiketi ya kuendelea kusonga  mbele katika hatua ya makundi Klabu Bingwa Afrika. 

Mchezaji wa kikosi hicho Ibrahim Ajibu Migomba  amesema kuwa matarajiao yao ni kuondoka na ushindi mnono huko ugenini ili kuendelea kusonga mbele zaidi. 

"Tumedhamiria kuondoka na ushindi  jumamosi ili tusonge mbele hatua ya makundi klabu bingwa Afrika Kikubwa dua na kudra za mwenyezi Mungu “amesema Ibrahim Ajibu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...