BENKI
ya BancABC imesema imetekeleza Sera ya fedha ya Benki Kuu ya
Tanzania(BoT) kwa kutangaza kutoa punguzo kwa wateja wake wapya
kuwezesha kukopa kuanzia Aprili 1 mwaka huu.
Akizungumza
leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji was BancABC Dana Botha
amesema benki hiyo ni sehemu ya Atlasi Mara iliyosajiliwa katika soko
la hisa la Londan ikiwa na lengo la kujitanua ili kuwa kinara katika
masuala ya kifedha katika ukanda wa Sahara kwa kutumia uzoefu wake na
uwezo wa kukuza mitaji.
Hivyo
Botha amesema watapungunza riba kwa wateja wao katika mikopo ya
masharti ambayo itakuwa ni huduma ya Over draft pamoja na ya nyumba na
kufafanua mwaka jana benki nyingi zilipita katika wakati mgumu wa
ukwasi.
"Hivyo
kufanya uwezo wa kukopesha kuwa mdogo.Kwa miezi kadhaa sasa,Serikali
kupitia BoT imekuwa ikisisitiza kuhusu punguzo la riba hiyo kwa
kupunguza masharti kama vile kiwango cha chini cha fedha kwa
mabenki,"amesema Botha.
Mkurugenzi mtendaji wa BancABC Dana Botha akizungumza na waandishi wa habali katika ofisi zao Leo Jijini Dar es Salaam,kuhusu punguzo la tozo ya mikopo mbali mbali kwa wateja wao.
Mkurugenzi Mtendaji wa BancABC Dana Botha kulia,kushoto ni Mkuu wa kitengo cha Hazina BancABC Barton Mwasamengo pamoja na Mkurugenzi wa kitengo cha wateja binafsi na wafanyabiashara wa BancABC Joyce Malai katikati wakishika bango linaloonyesha punguzo la tozo za Mikopo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...