Na John Nditi, Morogoro
UONGOZI wa Chuo  Kikuu  cha Waislamu cha Morogoro (MUM) kinatarajia kujenga kampasi  tawi la Kigamboni, Jijini Dar es Salaam  itakayo kutoa shahada mbalimbali za masomo ya usimamizi wa biashara na kwa kuanzia na udahili wa wanafunzi 5,000.

Chuo hicho  Kampasi ya  Kigamboni ni kuwezesha  kupata wataalamu wengi wa  usimamizi wa biashara watakaokidhi  mahitaji  ya soko la ajira katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki  pamoja na Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).

Makamu mkuu wa Chuo Kikuu hicho, Profesa Hamza Njozi,alisema  wakati wa uwekeji wa jiwe la msingi  kitakapojengwa eneo la Lingato , Kata ya Kisarawe II ,Manispaa ya Kigamboni , Jijini Dar es Salaam.

Profesa Njozi alisema, tangu kuanzishwa kwa Chuo hicho Oktoba 23, 2004 chini ya Mfuko wa Taasisi ya Maendeleo ya Waislamu (MDF) na kilizinduliwa rasmi Oktoba 22, 2005 na  Rais wa Serikali ya awamu ya tatu , Benjamin William Mkapa .

Makamu Mkuu wa Chuo hicho alisema, hadi  kufikia mahafali ya kumi mwaka jana ,kimeshatoa wahitimu 5,433 wa ngazi ya Shahada, Stashahada na Astashahada  ambapo  kwa sasa kina zaidi ya wanafunzi 3,000 na uwezo wa chuo ni kuchukua wanafunzi 8,000.

Profesa Njozi  alisema , kujengwa kampasi  Tawi la Kigamboni kunatarajiwa kuongeza udahili wa wanafunzi wa ndani na n je ya nchi baada  ya uongozi wa Chuo kupata  eneo la ardhi lenye  ukubwa wa ekari 400 kwa ajili ya ujenzi huo.
 Makamu mkuu wa Chuo  Kikuu  cha Waislamu cha Morogoro (MUM) , Profesa Hamza Njozi akipanda mti baada ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi  wa Kampasi yake  itakayo kutoa shahada mbalimbali za masomo ya usimamizi wa biashara itakayojengwa eneo la Lingato , Kata ya Kisarawe II, Manispaa ya  Kigamboni, jijini Dar es Salaam.
 Makamu mkuu wa Chuo  Kikuu  cha Waislamu cha Morogoro (MUM) , Profesa Hamza Njozi ( wapili kushoto  fulana pundamilia) akibadirishana mawazo na mmoja wa viongozi wa Chuo hicho baada ya  uwekaji jiwe la msingi la ujenzi  wa Kampasi ya Kigamboni  itakayo kutoa shahada mbalimbali za masomo ya usimamizi wa biashara itakayojengwa eneo la Lingato , Kata ya Kisarawe II ,Manispaa ya  Kigamboni, jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wanafunzi  wakiume  wa Chuo  Kikuu  cha Waislamu cha Morogoro (MUM) wakisaidia kubeba tofari  hadi eneo la  uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi  wa Kampasi  ya Kigamboni  itakayo kutoa shahada mbalimbali za masomo ya usimamizi wa biashara itakayojengwa eneo la Lingato , Kata ya Kisarawe II ,Manispaa ya  Kigamboni, jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya Wanafunzi wakike wa Chuo  Kikuu  cha Waislamu cha Morogoro (MUM)  wakisaidia kusogeza mfuko wa saruji kwa ajili ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi  wa Kampasi  yake itakayo kutoa shahada mbalimbali za masomo ya usimamizi wa biashara itakayojengwa eneo la Lingato , Kata ya Kisarawe II ,Manispaa ya  Kigamboni, jijini Dar es Salaam.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...