Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii.
MALKIA wa muziki wa Bongo fleva nchini, Judith Wambura a.k.a Lady Jaydee ametaja majina ya wasanii wengine watakaomsindikiza katika Tamasha la  Unaweza linalotarajia kufanyika Machi 31 mwaka  katika Hotel ya Golden Tulip Ostetbay.

Akizungumza na Michuzi blog Jaydee amewataja wasanii hao ni Bushoke, Nick Mbishi, Alawi Junior na Wengine wengi.

"Hii ni shoo ambayo nataka kila mtu afurahie muziki akiwa nyumbani na ladha ambazo walikuwa wamezikosa kwa muda mrefu, hivyo kupitia onesho hilo nitaka kiu yao ya kutonusikia kwa muda kidogo," amesema Jaydee

Aidha mwanamuziki huyo amesema siku hiyo kutakuwa na watu maarufu akiwamo MC Pilipili na wengine wengi.

Amesema maandalizi ya shoo hiyo yamekamilika na kwamba amejiandaa vya kutosha.

Amefafanua shoo hiyo itaanza  saa12 jioni ambapo Machozi Band watakuwa jukwaani na kumalizika  saa  sita usiku atamaliza lakini ana uhakika watakaofika watakuwa wameandika historia ya aina yake kutokana na namna alivyojiandaa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...