Na
Koleta Njelekela, Stamico Dar Es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji mpya wa STAMICO Kanali Sylivester Damian Ghuliku amekabidhiwa rasmi Ofisi na aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa STAMICO Mhandisi John Nayopa na kuanza kazi rasmi tarehe 05 Machi, 2018.
Makabidhiano hayo yamefanyika Makao Makuu ya STAMICO yaliyopo barabara ya Umoja wa Mataifa, Upanga jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya STAMICO Balozi Alexander Muganda.
Akizungumza katika hafla hiyo fupi ya makabidhiano, Mhandisi Nayopa amesema STAMICO inajukumu kubwa la kusimamia rasilimali za madini kwa niaba ya Serikali pamoja na kuwekeza katika Miradi ya Kimkakati ya Uchimbaji Madini, ili kuongeza mchango wa madini katika Pato la Taifa.
Amemshauri Kanali Ghuliku kuendeleza ushirikiano na Serikali, Wizara ya Madini na wadau katika kutekeleza miradi ya ubia na isiyo ya ubia; kuendesha kampuni zake tanzu na kuendeleza leseni za uchimbaji pamoja na shughuli za wachimbaji wadogo.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa zamani wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mhandisi John Nayopa (kulia) akimkabidhi taarifa ya Utendaji Kazi ya Shirika Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Mpya wa Shirika hilo Kanali Sylivester Damian Ghuliku(kushoto) katika hafla fupi iliyofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya STAMICO zilizoko jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji mpya wa STAMICO, Kanali Sylivester Damian Ghuliku akiwa katika picha ya pamoja Viongozi wa STAMICO na Wafanyakazi mara baada kukabidhiwa ofisi hiyo tayari kwa kuanza utekelezaji wa majukumu ya STAMICO.
Mkurugenzi wa Rasilimali watu na Utawala wa STAMICO, Deus Magala(kushoto) akikabidhi Clients Service Charter ya Shirika kwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji mpya wa STAMICO, Kanali Sylivester Damian Ghuliku(kulia) mara baada ya Kiongozi huyo kukabidhiwa ofisi na kusaliamiana na Wafanyakazi.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...