Balozi wa Tanzania Nchini Rwanda  Mhe.Ernest Mangu na Meja Jenerali Mstaafu Simon Marco Mumwi  wa  Urusi leo wamekutana na kuzungumza na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan mjini Dodoma.

Mabalozi hao walifika kwenye makazi ya Makamu wa Rais, Kilimani Dodoma  kwa lengo la kumuaga ,walimuahidi Makamu wa Rais kufanya kazi kwa ajili ya Tanzania.

Wamemuambia Makamu wa Rais wanajua dhamana kubwa waliopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na dhamira yake ya Tanzania ya Viwanda .
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Urusi Mhe. Jenerali Mstaafu Simon Marco Mumwi pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Rwanda Mhe. Ernest Mangu ambao walifika nyumbani kwa Makamu wa Rais kwa lengo la kumuaga kwenye makazi yake Kilimani mjini Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan(katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na  Balozi wa Tanzania nchini Urusi, Mhe. Jenerali Mstaafu Simon Marco Mumwi(kushoto) pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Rwanda, Mhe. Ernest Mangu(kulia) ambao walifika nyumbani kwa Makamu wa Rais kwa lengo la kumuaga kwenye makazi yake Kilimani mjini Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...